mrekebishatabia
Member
- Aug 20, 2014
- 10
- 13

Nampenda sana Millard Ayo nilijua ana kitu cha tofauti tangu anaanza kazi ya utangazaji.
Sio kwamba nilivutiwa na story yake aliyopitia.
Jamani anastahili credit nyingi sana.
Habahatish anaanda habari za uhakika, ataenda eneo husika, atatafuta wahusika hata kama ni mazingira hatarishi. Tunajua ana sauti nzuri angeweza kukaa tu lakini anaondoka ofisini kwake kutafuta habari.
Ataiandika habari, atapiga picha na kisha kutangaza. Nawaambia ukweli mwandishi wa namna hii kila mwaka atakuwa anachukua tuzo halafu unakuta wanaomuonea wivu wako busy kwenye social networks kutafuta habari. Jamani si mpaka uwe na elimu kubwa ndo ulete mabadiliko mahala pa kazi yako.
Tatizo sio mshahara hata kama ni mdogo watu wanaanzia chini ukiwa mwaminifu ukajituma kuanzia ngazi ya chini milango itafunguka mingi baadae. Mwandishi yeyote wa habari anayeamini anajituma kwenye kazi yake, awe mtangazaji, mpiga picha, blogger, mwandishi wa gazeti, katuni nk.
Unaamini kazi yake anaipenda na kuithamini.
Big up Millard Ayo na wote mnaoipa sifa Tanzania kwa uandishi bora.