Namshauri Mo Dewji aivunje Bodi ya Wakurugenzi Simba, imejaa wajanja wajanja wengi wanahujumu timu

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
390
Reaction score
1,425
Namshauri Mo Dewji, kama kweli anataka kuendelea kuona mafanikio Simba basi hana budi kuvunja bodi ya wakurugenzi, hao akina Asha Baraka, sijui Mangungu, sijui Kaduguda hawana msaada wowote, hao ni watu ambao machoni ni kama watu lakini mioyoni mwao wenzetu.

Namshauri Mo Dewji asije kuweka Bilioni 20 zake, atakuja kulia, mipango ni mingi sana ya ujanja ujanja, ndio maana nasema Ceo Barbra akae pembeni kulinda heshima yake, timu hizi haziwez kuendelea had siku ya kiama, ondoa wajumbe waswahili wote ndani ya bodi, narudia vunja bodi ya wakurugenzi, haina msaada kabisa kabisa kwa maslahi ya timu hiyo.

Wakizingua waachie timu yao.
 
Kaduguda juzi alisema kwenye redio hataenda Mwanza maana simba wanafungwa, alijuaje?
 
Kaduguda juzi alisema kwenye redio hataenda mwanza maana simba wanafungwa, alijuaje?
Kweli wewe ulikuwa unaamini Simba atashinda kwa kikosi kile? Msimu huu Simba hawapo vizuri usimhisi tofauti Mzee.
 
Yanga ilivokuwa mbovu ilimchapa simba. Ulitegemea yanga ikiwa imara kabisa ifungwe na simba? Ni bahati tu hamjala khamsa.
 
Aivunje bodi kweni yeye ndio ameiteua, hiyo ni kazi ya wanachama
 
Kabisaaa yaan, huwa anapiga had panaoza. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ni Raha sana mwanaume kupiga kagoli kamoja acha mwanamke ahangaike na manne yake


[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Magazeti yaliandika

-Kwa Kocha huyu Simba vilio basi
-Kocha wa makombe atua Msimbazi
-Kwa Kocha huyu,Kila mechi Simba itaua tu

NB: Mashabiki wa Simba kumbebesha Pablo zigo la Misumari ni kumuonea, makosa yalifanyika na viongozi wa Simba ilikuwa kamari sana kumleta mtu ambaye hajawahi kufundisha mpira Africa na hajui chochote kuhusu soka la Africa,tena katikati ya msimu......hawajui wachezaji wake vizuri ndiyo maana mpaka leo hana first eleven.Pili,mlifail sana kwenye usajili wa wachezaji mfano Sakho, Kanoute,Banda type ya wachezaji hawa wapo Bongo wengi tu......mlifaulu Kwa yule anayemkamia Mayele tu.......Sakho atakupa kitu game moja kati ya 5,hana tofauti na Morrison ni wachezaji wa majukwaa ila hawana msaada na timu ikiwahitaji.
 
Mwendesha baiskeli wa makolo ana goli mbili NBCPL
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…