Namtaka Singo maza

Namtaka Singo maza

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
893
Reaction score
1,021
NAMTAKA SINGO MAZA

1 Nimehangaika sana, kuyatafuta mapenzi
Niliowapa amana, hata hawakuienzi
Nikapigwa dana dana, na kufanyiwa ushenzi
Namtaka singo maza, ndie nitayemuoa

2 Aloumizwa ja mimi, huenda tukalandana
Hatusikizi akwami, wawili tukipendana
Tukuze wetu uchumi, mawazo kuliwazana
Namtaka singo maza, ndie nitayemuoa

3 Kapita mingi mishale, hataogopa umande
Ajua haya na yale, kwa juhudi ajipinde
Mjuzi mambo ya kale, kucheza ngoma sikinde
Namtaka singo maza, ndie nitayemuoa

4 Asiwe mwingi wa wana, hapo hapatanifaa
Ukimwona kama mwana, hutadhani kashazaa
Awe mmoja wa ujana, ndoa tutaiandaa
Namtaka singo maza, ndie nitayemuoa

[emoji3578]Abuuabdillah
Whatsapp 0744883353
[emoji338] 0718569091
jumaomari5@gmail.com
Moshi- Kilimanjaro
 
Namtafuta mchumba


1 Hodi naleta maombi, ya uchumba
Hapa niiweke kambi, na kulimba
Nile za maziwa tambi, nina sumba
Namtafuta mchumba, ajilani


2 Barua hii iwazi ,isomeni
Na awe yangu saizi, mleteni
Wajulisheni wazazi, dalihini
Namtafuta mchumba, ajilani

3 Rangi sitazichagua, auswadi
Na wala sitamgua, niafidi
Nami nitamchungua, nifaidi
Namtafuta mchumba, ajilani

4 Kiuno kiwe dondora, ajimali
Abadi sitamsora ,mi hamali
Anivalie na gora , ni ulili
Namtafuta mchumba, ajilani

5 Niufunge ukurasa, wa kitabu
Awe banati kisasa, sitasubu
Kwake yeye 'tajinasa, niwe dubu
Namtafuta mchumba,ajilani


[emoji2399]Abuuabdillah[emoji1614]
Whatsapp 0744883353
Moshi -- Tanzania
 
NAMTAKA SINGO MAZA

1 Nimehangaika sana, kuyatafuta mapenzi
Niliowapa amana, hata hawakuienzi
Nikapigwa dana dana, na kufanyiwa ushenzi
Namtaka singo maza, ndie nitayemuoa

2 Aloumizwa ja mimi, huenda tukalandana
Hatusikizi akwami, wawili tukipendana
Tukuze wetu uchumi, mawazo kuliwazana
Namtaka singo maza, ndie nitayemuoa

3 Kapita mingi mishale, hataogopa umande
Ajua haya na yale, kwa juhudi ajipinde
Mjuzi mambo ya kale, kucheza ngoma sikinde
Namtaka singo maza, ndie nitayemuoa

4 Asiwe mwingi wa wana, hapo hapatanifaa
Ukimwona kama mwana, hutadhani kashazaa
Awe mmoja wa ujana, ndoa tutaiandaa
Namtaka singo maza, ndie nitayemuoa

[emoji3578]Abuuabdillah
Whatsapp 0744883353
[emoji338] 0718569091
jumaomari5@gmail.com
Moshi- Kilimanjaro
MaashaAllah
 
Back
Top Bottom