Ki ukweli ndugu yetu huyu tunamtetea tu, lakini uwezo wake hauridhishi. Na sio mchezaji wa kwanza kutoka Genk kwenda EPL na kukutana na changamoto anazokutana nazo yeye.
Kuna mtu anaitwa Kevin De Bruyne alichukuliwa na Mourinho kutoka Genk akaenda Chelsea kwa ada ya Pound Mil 8, January 2012. Baadaye Mou akaona kama KDB uwezo wake mdogo akamtoa kwa mkopo kule Werder Bremen, Germany. Jamaa akakiwasha sana kule Germany mpaka Klopp (akiwa Dortmund) akataka kumchukua lakini Mou akamzuia kwenda, akamwambia bado ana mipango naye. Na alinukuliwa kocha wa Werder Bremen (Thomas Schaaf) akisema wangeshuka daraja kama sio juhudi binafsi za Kevin De Bruyne. Ilikua msimu wa 2012/2013.
Lakini KDB alivyorudi Chelsea akacheza game kama tatu tu halafu Mou akaanza kumpiga Bench tena karibu msimu mzima. KDB akaona isiwe tabu akamuomba Mou kwa huzuni sana kuliko aendelee kusugua Bench bora tu amuuze kule Bundesliga mazima maana anaona kama Chelsea haina mipango nae. Anaonekana kiwango chake ni duni.
Mou akaamua kumtupia Wolfburg kwa pound Mil 22, January 2014 kama garasha lililoshindwa kumridhisha. Lakini jamaa akaenda kukiwasha mbaya kabisa kule Bundesliga na kuchukua uchezaji bora huku akiweka assists record (2014/2015). Akiwa Wolfsburg, Offer zikamininika kutoka PSG, Bayern na Man City lakini yeye akaona kwa aina ya mpira anaocheza, Man City ndio itamfaa. Na August 2015, akauzwa kwenda Man City kwa kitita cha Pound Mil 76.
So, Chelsea walimuona hafai kama anavyoonekana Samatta Aston Villa. Lakini KDB hakukata tamaa mpaka leo hii ni miongoni mwa wacheza bora kabisa pale EPL. Na anakaribia kuvunja rekodi ya assists ya Thierry Henry. So samatta needs to deliver outstanding performance bila hivyo watamnyoa siku si nyingi.
Wazungu hawana huruma na mtu asiyeleta mabadiliko kwenye timu. Asijifariji kuwa sababu ya kutokufunga magoli ni kutokupewa pasi na na wachezaji wengine. Atatimuliwa asipojiongeza kujua namna bora ya kucheza epl na kupata matokeo. Kila la Kheri kwake. Akazane!
Ni mtazamo tu!