Jinsi mwenendo wa Katiba mpya unavyoenda, kuna uwezekano ikachelewa kukamilika na kuundwa kwa tume huru kwa ajili ya Uchaguzi wa 2015!!!!
Mbaya zaidi, Tanzania inakabiliwa na matatizo makubwa ya ufisadi, Ujinga/Elimu duni, Afya Mbaya, na Unga/Levya. Haya matatizo hayatatuliki kwa serikali ya sasa na haya matatizo yanazidi kuwa sugu kwa sababu hakuna hatua mujarabu zinachukuliwa.
Kuna mambo mengi yanaendelea, Suala moja gumu ni Muungano, suala la Tanganyika na Muswada wa katiba.
Bila kuwa na maelewano ya dhati kati ya vyama na maridhiano ya wananchi, hatutapata Katiba mpya kwa wakati.
Ni lazima yawepo masikilizano, ubabe haitakuwa na maana..... kutumia nguvu ya Dola ni umbumbumbu
Pendekezo la Bwana Kibamba (Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba) linaungwa mkono. Tume ya sasa ivunjwe na sasa iundwe tume Huru ya uchaguzi kwa ajili ya Kuboresha daftari la wapiga kura, kusimamia kura ya maoni kama tuwe na Tanganyika ama la na kusimamia uchaguzi serikali za mitaa 2014 na Uchaguzi mKuu 2015.
Mapendekezo/Maoni ambayo yametolewa katika kuunda katiba mpya, yaingizwe katika katiba ya sasa ili kuunda tume Huru ya UChaguzi.
Tume huru iwe na wajumbe huru ifuatavyo.
- Vyama vya siasa
-Jukwaa la katiba
-NGOs
-Dini zote
-Vyuo.
Nawasililisha ili wana JF mujadili na kutoa maoni nini kifanyike.
Mbaya zaidi, Tanzania inakabiliwa na matatizo makubwa ya ufisadi, Ujinga/Elimu duni, Afya Mbaya, na Unga/Levya. Haya matatizo hayatatuliki kwa serikali ya sasa na haya matatizo yanazidi kuwa sugu kwa sababu hakuna hatua mujarabu zinachukuliwa.
Kuna mambo mengi yanaendelea, Suala moja gumu ni Muungano, suala la Tanganyika na Muswada wa katiba.
Bila kuwa na maelewano ya dhati kati ya vyama na maridhiano ya wananchi, hatutapata Katiba mpya kwa wakati.
Ni lazima yawepo masikilizano, ubabe haitakuwa na maana..... kutumia nguvu ya Dola ni umbumbumbu
Pendekezo la Bwana Kibamba (Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba) linaungwa mkono. Tume ya sasa ivunjwe na sasa iundwe tume Huru ya uchaguzi kwa ajili ya Kuboresha daftari la wapiga kura, kusimamia kura ya maoni kama tuwe na Tanganyika ama la na kusimamia uchaguzi serikali za mitaa 2014 na Uchaguzi mKuu 2015.
Mapendekezo/Maoni ambayo yametolewa katika kuunda katiba mpya, yaingizwe katika katiba ya sasa ili kuunda tume Huru ya UChaguzi.
Tume huru iwe na wajumbe huru ifuatavyo.
- Vyama vya siasa
-Jukwaa la katiba
-NGOs
-Dini zote
-Vyuo.
Nawasililisha ili wana JF mujadili na kutoa maoni nini kifanyike.