Namwachia nyumba mama mkwe

na ikitokea hao wakwe ndo 'wazazi' wa Esperance anakimbilia wapi sasa?<br />
<br />
tukiachilia mbali hiyo mitishamba na kabila lako, Esperance huna tatizo lingine na mkwe wako? huwezi kuwa pia na wewe unachangia kwenye shida ya hiyo ndoa yako?
<br />
<br />
ugomvi ulianzia kwa mtoto wangu, alimnyoa nywele kidogo, nikahoji akasema mimi sio kbila lao siwez kujua mambo hayo. Vita akaanzia hapo me sio wa kwanza kwenye hyo familia kukutwa na hayo.
 
Sweetheart unajua ile Women to women talk ,
Hebu funga mkanda umuombe mama mkwe kuongea nae mkiwa wawili tu hata Housegal asiwepo kutoa ushahidi,baada ya hapo mwambie akupe ukweli wake kuhusu wewe,
Kama hakupendi mwambia ndo Choice ya mwanae
Kama anakufundisha ulozi mwambie ..wewe unamwamini mwenyezi mungu pekee
Hapa ndo hekima yako inatakiwa kwa huyo mama mkwe.
Ukiona haelewi somo Esperance kapumzike kwenu mpaka mmeo aje kutatua hii migogoro .....
 
Esperance ....mumeo lazima achukue maamuzi sahihi na magumu. He shpuld face her mother and tell it to her face to stop doing what she is doing! Kitaalaamu (at least what have read here and there) huyo jamaa hajakua, bado yuko katika kipindi kile tukiwa watoto tunaamini wazazi wetu wana akili sana, hawakosei na wanajua kila kitu. Wewe pia kama mkewe msaidie kumtoa usingizini, usimhukumu, anahitaji msaada wako. Kama wote mnapendana kwa dhati msaidie, mpe nifano kama unayo kuhusu wewe unavyokabiliana na wazazi wako. Lazima ajue kuwa wazazi watawaacha (tukifuata natural course tunategemea wazazi watakufa kabla ya watotot wao, sio?) sasa akikaa anamsikiliza mama yake atapoteza ndoa yake kwa uoga wake na siku mama yake akifariki (sio uchuro) na kujusikia kuwa yu huru sasa itakuwa too late, pengine hautakuwa unamsubiri. Binafsi nimeshakuwa katika situation kama hiyo, na nilishinda, I chose my wife over my mother! inataka UJASIRI!
 
Saa nyingine hata nyie wake zetu mna matatizo bana, hivyo mi sikuamini 100% kwamba mama mkwe ndo mbaya. Jitoe kwanza boriti jichoni mwako.
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
ndg shukuru kama mamako ni mwelewa, haiwezekani watoto wote wa kiume 4 wake zao tuwe wabaya. Mama anaweza kukaa kwako miez 6 haumwi wala nini na kwake ni hapa hapa mjini na sio kama hajiwezi. Na kubagua wajukuu ambao sie wanawake sio wakabila lake??
 

FL1...uko sahihi kabisa hii pia inaweza kuwa njia sahihi, nyie wawili tu, sababu kama kukiwa na mtu wa tatu, kwa aiubu ataleta ubishi na hatakubali kukusikiliza. Mtafutie siku , wawili tu. Unaweza kumfuata chumbani ukafunga mlango na kumwambia akueleze tatizo ni nini, Openly mwambie umechoka na mambo yake, anakukera, na kuwa hapo ni kwako hautaondoka. Jamaa mekuzimia na yeye hana jinsi ya kuibadilisha hiyo.....in short mpe Mkwara wa nguvu lakini uliojaa facts tupu!
 
<br />
<br />
thanx, hii nilikuwa sijaijaribu dear. Point taken.
 
Ningekuwa mimi hata nisingesubiri chochote as long as pande zote wanafahamu hayo matatizo ni mbio kwa mama yangu kha!!

Maana nakumbuka ulishaleta malalamiko kama haya naona ugonjwa unakomaa sasa.

Pole nenda kwenu kapumzike hatukuja duniani kuteseka bana!!! Subiri mumeo aje muendelee na maisha
 

te te te DA bana
 
<font color="#800080"><font size="4"><span style="font-family: comic sans ms">Esperance my dear....sina uzoefu na mambo hayo kivile....lakini nakushauri nenda kapumzike kwa mama yako mpaka mmeo arudi.....khaaa!!....</span></font></font>
<br />
<br />
sijaoa, sina uzoefu wa ndoa, ila naunga mkono uamuz wako. BUT Make sure unamtaarifu mumeo kuhusu uamuz wako wa kuondoka na sababu ya kuondoka ili isilete tafsiri tofaut. Pole
 
umeshanunua solex au bado unajibu hoja humu?
 
..Ndoa ni Uvumilivu Dada yangu, Jaribu kuvumilia na kama ni muumini mzuri wa Dini, piga magoti kila siku Usali umwambie Mungu shida zako, Mungu ni muweza, anaweza, atayamaliza. Hebu fikiria utakapo rudi nyumbani nini kinatokea, Watoto wako hawana kosa utawaacha, Mume wako bado unampenda utamuacha.
Vumilia yana Mwisho hayo.
 
Kwani kwenu umeua unaogopa kurudi??? Kajipumzikie zako bana
 
Komaa, akimwaga mboga mwaga ugali. Ndo maisha ya cku hizi. Kuishi na wanadamu kazi. Yataka kifua mdogoangu. Komaa.
 
Mimi ningemwitia watoto wa afande mwema.si ana kwake jamani?Na inajulikana kuwa ni mkorofi.mwitie police.mme wako mweleze ukweli then ongeza na chumvi.
 
Kwani kwenu umeua unaogopa kurudi??? Kajipumzikie zako bana

ni wazo zuri ila angempigia mr wake simu halafu akasepa au angempa live bi mkubwa kuliko kufa kijurumani na tai shingoni.
kweli ndoa ndoano..
 
dada nakuomba sana uongee na mmeo umweleze suala la uhamaji wako hapo nyumbani na umweke wazi uko tayari kurudi kwako akirudi yeye
 
Mimi ningemwitia watoto wa afande mwema.si ana kwake jamani?Na inajulikana kuwa ni mkorofi.mwitie police.mme wako mweleze ukweli then ongeza na chumvi.

Ha ha ha ha nimecheka kwa nguvu kweli kha??
 
<br />
<br />
Mlete baba yako hapo nyumbani ili wamalizane kiutu uzima, huyo mama ana LIBIDO
 
komaa nae huyo-hadi yeye achemshe-kumkimbia ni kumpa ushindi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…