bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,679
Abdi Kasim babi ndio ni mmoja wa mafundi wa soka kutokea Zanzibari akibebwa na nguvu/stamina pamoja na ukali wa mashuti yake.
Abdi Kasimu amecheza Yanga kwa mafanikio makubwa na alikua kati ya wachezaji tegemeo wa Yanga kipindi kile, Pia amecheza T/Stars na Zanzibar Heroes kwa kiwango kikubwa ni mchezaji aliyestaafu na mpira wake.
Leo hii kuna kijana mwingine Fundi kabisa kutoka kule kule Zenji wakuitwa Shekhani Ibrahimu aliyesajiliwa na Yanga msimu huu kijana naye anapita mule mule kwa Abdi Kasimu kijana ana uwezo mkubwa wa kupiga ndani ya 18 na nje ya 18 ukitaka kuuliza muulize Kipa wa APR ya Rwanda.
Baada ya Kijana kuingia kipa wa APR alikua ana kazi nzito ya kufanya uokozi wa michomo hatari kutoka kwa Kijana Shekhani na huku moja ikigonga mwamba wa juu.
Miguu ya Kasimu Babi imerudi tena pale Jangwani, sina shaka na wachezaji kutoka Zenji wanajua sana kujitunza na kuwa na mwisho mzuri kwenye Soka.
Pale Jangwani kijana akiongezewa vikitu vichache tu vya kimpira, kujitunza na nidhamu hakika atakua mchezaji wa tegemeo wa Yanga mbali na sifa za Ukasimu ndani yake pale ana Uacho ndani yake sema kamshinda kidogo Dr Aucho kwa mishuti yake ile.
Namwona kijana mbali zaidi .
Roma ikisema imesema.
Abdi Kasimu Babi
Shekhani Ibrahimu
Abdi Kasimu amecheza Yanga kwa mafanikio makubwa na alikua kati ya wachezaji tegemeo wa Yanga kipindi kile, Pia amecheza T/Stars na Zanzibar Heroes kwa kiwango kikubwa ni mchezaji aliyestaafu na mpira wake.
Leo hii kuna kijana mwingine Fundi kabisa kutoka kule kule Zenji wakuitwa Shekhani Ibrahimu aliyesajiliwa na Yanga msimu huu kijana naye anapita mule mule kwa Abdi Kasimu kijana ana uwezo mkubwa wa kupiga ndani ya 18 na nje ya 18 ukitaka kuuliza muulize Kipa wa APR ya Rwanda.
Baada ya Kijana kuingia kipa wa APR alikua ana kazi nzito ya kufanya uokozi wa michomo hatari kutoka kwa Kijana Shekhani na huku moja ikigonga mwamba wa juu.
Miguu ya Kasimu Babi imerudi tena pale Jangwani, sina shaka na wachezaji kutoka Zenji wanajua sana kujitunza na kuwa na mwisho mzuri kwenye Soka.
Pale Jangwani kijana akiongezewa vikitu vichache tu vya kimpira, kujitunza na nidhamu hakika atakua mchezaji wa tegemeo wa Yanga mbali na sifa za Ukasimu ndani yake pale ana Uacho ndani yake sema kamshinda kidogo Dr Aucho kwa mishuti yake ile.
Namwona kijana mbali zaidi .
Roma ikisema imesema.
Abdi Kasimu Babi
Shekhani Ibrahimu