Nani alaumiwe?

Nani alaumiwe?

Remmy

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2009
Posts
4,701
Reaction score
1,803
jamani wana jamii naombeni msaada wenu wa dhati kabisa. nilikuwa na mchumba mtarajiwa kabisa wa kuwa mume wangu, tumekuwa kwenye urafiki kwa mwaka na nusu sasa, nimeenda kwa wazazi wake na nduguze wananifahamu kabisa na kunipenda. ikatokea kutokuelewana kati yangu na huyo jamaa kwasababu alificha mambo ya msingi, kwanza alibadilika na kuwa mlevi sana, hakuwa akitambua wajibu wake yeye maisha ilikuwa bora liende, hakuwa muelewa kabisa but kabla alikuwa so sweet, understanding u cant imagine na alikuwa mlokole wa assemblise of God baadae akaasi na kuwa hivyo mlevi, then ikaja julikana huyo jamaa ana watoto watatu kwa mama wawili tofauti, yaani alishawahi kukaa na wake wawili kabla akashindwana nao mie nilikuwa watatu bila kujua so baada ya kutambua hayo si nikaona huyu mwanaume hanifai nikaamua kubreak relation, jamaa akatuma sms kwa ndugu zake kuwa anajiua kwasababu mie nimemkataa jamaa si amejiua kweli na lawama za ndugu na jamii yote iko kwangu. naombeni msaada wanafanya sahihi kunihukumu mimi, je na ni kweli nimechangia kifo chake kwa kumkataa, nipo nimekata tamaa sana mie najiona sina hatia kwasababu hakuwa muwazi, na siku ya msiba hao watoto walikuwepo. ndugu hao walificha yote waliyoyafahamu kuhusu huyu jamaa. MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA PEPONI... AMEN
 
Back
Top Bottom