MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 707
Ndugu Wanabodi,
Baada ya kutokea kwa mabadiliko ya hali ya hewa, yaliyoambatana na ukame uliosababisha, mnamo mwaka 1994, mgao wa umeme ulioisababishia Tanzania athari kubwa ya kiuchumi, kwani watu wengi walipata hasara kubwa, binafsi nilidhani lingetokea jopo la wataalam, kama vile wachumi na wanasayansi, ambao wangeishauri Serikali nini ifanyike, ili hata kama hali hiyo mbaya ya hewa ikijirudia, hatua za dharura ziwe zimekwishaandaliwa.
Jambo hilo halikufanyika. Matokeo yake, ukaja ufisadi wa Richmond na majeraha mengine ya vita hii kali ambayo sitaki kuyataja hapa, kwa kuhofia kutonesha vidonda vyenu.
Swali ninalouliza ni, baada ya kukabidhi madaraka ya utawala kwa Serikali, ye, tulikabidhi pia madaraka ya kufikiria? Jambo hili halikuhitaji mtu apewe ruksa ya kufikiria nini kifanyike, wala kuitwa atoe ushauri wake. Lilihitaji mtu, kama mtaalam, mwanasayansi - fizikia, uhandisi, elektroniki, mazingira, umeme, n.k. - ajitokeze na kusema nini kifanyike. Aandaye Mkakati Kazi, ambao ungefuatwa na Serikali, au ungekabidhiwa kwa Wajasiriamali/Wawekezaji wa Ndani, ambao wangeutekeleza.
Wote mmejionea jinsi ambavyo TANESCO imeshindwa kufanya kazi yake. Haina wataalam wa kutosha, waliopo wamechoka hata akili zao. Najua baadhi yao wamo humu, wataona ninawaone. Lakini niwaulize. Je, umeme unazalishwa kwa njia moja tu, yaani ya kutumia nishati itokanayo na bidhaa za petroli (dizeli, gesi, n.k.)? Mbona hata siku moja sijawasikia wataalam wa TANESCO wakishauri njia mbadala za kuzalisha umeme zitumike, kama vile nguvu za upepo, au teknolojia ya Stirling (ambayo imezuiwa makusudi na Serikali ya Marekani pamoja na Jumuiya ya Ulaya, kwani itaiwezesha nchi hii kuacha kuagiza mafuta au kuchimba gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme)?
Kwa mtazamo wangu, umefika wakati Watanzania (wazawa) waanzishe shirika mbadala la umeme, ambalo litatumia njia mbadala za kuzalisha umeme, likianzia na nguvu za upepo. Kampuni kubwa kama vile Suzlon na Vestas zimetengeneza wind turbines zenye uwezo wa kuzalisha 3.0 MegaWatt kila moja. Vestas wamefanikiwa kufikia kiwango cha 3.0 MegaWatts, zikinunuliwa 10 tu, hizo ni 300 MegaWatts, ambazo zinaweza kutosheleza kwa sehemu kubwa ya Tanzania Bara au hata Zanzibar yote!
Ninawaomba wataalam wa Uhandisi wa Umeme wawasiliane nami kwa njia ya simu - 0786-019019 - ili tuanze Mkakati Kazi binafsi, wa kuangalia jinsi ya kusonga mbele.
Penye Nia pana Njia, na Umoja ni Nguvu, bila kusahau, Kidole Kimoja Hakivunji Chawa!
Tusikubali nchi hii kuwekwa rehani na mafisadi wa Dowans, Richmond, Songas na IPTL!
./Mwana wa Haki
Baada ya kutokea kwa mabadiliko ya hali ya hewa, yaliyoambatana na ukame uliosababisha, mnamo mwaka 1994, mgao wa umeme ulioisababishia Tanzania athari kubwa ya kiuchumi, kwani watu wengi walipata hasara kubwa, binafsi nilidhani lingetokea jopo la wataalam, kama vile wachumi na wanasayansi, ambao wangeishauri Serikali nini ifanyike, ili hata kama hali hiyo mbaya ya hewa ikijirudia, hatua za dharura ziwe zimekwishaandaliwa.
Jambo hilo halikufanyika. Matokeo yake, ukaja ufisadi wa Richmond na majeraha mengine ya vita hii kali ambayo sitaki kuyataja hapa, kwa kuhofia kutonesha vidonda vyenu.
Swali ninalouliza ni, baada ya kukabidhi madaraka ya utawala kwa Serikali, ye, tulikabidhi pia madaraka ya kufikiria? Jambo hili halikuhitaji mtu apewe ruksa ya kufikiria nini kifanyike, wala kuitwa atoe ushauri wake. Lilihitaji mtu, kama mtaalam, mwanasayansi - fizikia, uhandisi, elektroniki, mazingira, umeme, n.k. - ajitokeze na kusema nini kifanyike. Aandaye Mkakati Kazi, ambao ungefuatwa na Serikali, au ungekabidhiwa kwa Wajasiriamali/Wawekezaji wa Ndani, ambao wangeutekeleza.
Wote mmejionea jinsi ambavyo TANESCO imeshindwa kufanya kazi yake. Haina wataalam wa kutosha, waliopo wamechoka hata akili zao. Najua baadhi yao wamo humu, wataona ninawaone. Lakini niwaulize. Je, umeme unazalishwa kwa njia moja tu, yaani ya kutumia nishati itokanayo na bidhaa za petroli (dizeli, gesi, n.k.)? Mbona hata siku moja sijawasikia wataalam wa TANESCO wakishauri njia mbadala za kuzalisha umeme zitumike, kama vile nguvu za upepo, au teknolojia ya Stirling (ambayo imezuiwa makusudi na Serikali ya Marekani pamoja na Jumuiya ya Ulaya, kwani itaiwezesha nchi hii kuacha kuagiza mafuta au kuchimba gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme)?
Kwa mtazamo wangu, umefika wakati Watanzania (wazawa) waanzishe shirika mbadala la umeme, ambalo litatumia njia mbadala za kuzalisha umeme, likianzia na nguvu za upepo. Kampuni kubwa kama vile Suzlon na Vestas zimetengeneza wind turbines zenye uwezo wa kuzalisha 3.0 MegaWatt kila moja. Vestas wamefanikiwa kufikia kiwango cha 3.0 MegaWatts, zikinunuliwa 10 tu, hizo ni 300 MegaWatts, ambazo zinaweza kutosheleza kwa sehemu kubwa ya Tanzania Bara au hata Zanzibar yote!
Ninawaomba wataalam wa Uhandisi wa Umeme wawasiliane nami kwa njia ya simu - 0786-019019 - ili tuanze Mkakati Kazi binafsi, wa kuangalia jinsi ya kusonga mbele.
Penye Nia pana Njia, na Umoja ni Nguvu, bila kusahau, Kidole Kimoja Hakivunji Chawa!
Tusikubali nchi hii kuwekwa rehani na mafisadi wa Dowans, Richmond, Songas na IPTL!
./Mwana wa Haki