Nani anayekagua na kudhibiti ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG)?

Hukaguliwa na kampuni ya kimataifa itakayochaguliwa baada ya kushinda tenda
 
Kila mwaka huo nasikia ripoti za CAG Juu ya mapato, matumizi na utendaji ndani ya Serikali. Lakini sijawahi kusikia ripoti inayoonesha mapato, matumizi na utendaji ndani ya Ofisi ya CAG.

Je, nani hukagua Ofisi hii, na Je ripoti huwa zinapelekwa wapi?
 
Independent auditor. Not from the government say pwc,delloite etc and is appointed periodically by trasurer if I recall correctly
 
Kwa hili la rushwa naona lipo karibu na ukweli, na je, PCCB kwa rushwa???????
 
NAOT/CAG hukaguliwa na kampuni binafsi ya ndani au ya kimataifa na report yake hupelekwa bungeni kabla ya kuanza vikao vya ndani vya kamati za bunge la bajeti
 
Kuna external auditors wanawakagua kila mwaka,mara nyingi ni makampunu ya Afrika Kusini na Uingereza
Ofisi ya mkaguzi mkuu hukaguliwa na makampuni ya humu humu ndani na uteuzi wake husimamiwa na kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali
 
Namshukuru CAG kwa kuibua mambo kadhaa yenye msingi na yenye kuleta hoja katika jamii.
Nashukuru kwa serikali kuweka chombo hiki ambacho bila shaka kinadhibiti utendaji wa Serikali na kuzilinda rasilimali zetu katika hali zote.

Ila mimi kama mwananchi na mtendaji serikalini ambaye niliwahi kukutana na watendaji wenzangu kutoka ofisi ya CAG nina kila haki ya kuulizia swali hili.

Je ni nani anayemdhibiti CAG?

Ni nani anayemkagua CAG na ofisi yake?

Ni nani haswa anayetakiwa kumuuliza CAG juu ya ripoti anayoamua kiiwasilisha kama final report?

Je ni kivipi tunaweza kuikubali au kuikataa ripoti ya CAG kama watendaji?

Haya ni baadhi ya maswali yanayostahili majibu kutoka kwa CAG au wenye mamlaka ya tafsiri sahihi ya ripoti za CAG...Hii inaitwa Checks n balance!!

Katika utendaji wangu wa kazi niliwahi kuexperience CAG akiandika hoja ya upotevu wa fedha simply because kuna kifaa cha dharura ya kumuokoa mama mjamzito asife kwa upungufu wa damu...yaani hoja ilikuwa ni kununua kifaa hicho bila kuwepo kwenye bajeti.Maelezo yangu kwa CAG OFFICERS kwamba hiyo ilikuwa ni dharura inayopelekea vifo au chaos katika jamii yalionekana ni maelezo ya kipuuzi na sio ya kitaalamu...yaani perspective ya CAG OFFICERS ilikuwa kwenye ukiukwaji wa taratibu tu na hawakujali udharura ,majadiliano ya wataalamu na hitimisho la kitaaluma kuhusu nia na matumizi ya fedha .
CAG Officers hawakubaliani na maelezo ya wataalamu ya jinsi fedha zilivyotumika hata kama zimetumika kwa maendeleo....Thisi is how they act...They act like Robots!!

Zipo hoja nyingi sana wanazoripoti kwa muktadha huu huu wa Urobot!!

Ndio maana ninauliza je ni nani anayemdhibiti CAG?

Kwa muktadha huu huu ninaweza kusema CAG inabambikia mapungufu kwa Serikali...kwa kuwa hakuna wa kumdhibiti na kumhoji!

Hoja huwa zinajibiwa ila ni yeye ambaye huamua kuwa hoja imejibiwa au la...HAYA NI MAPUNGUFU.

Je CAG Apewe rungu la kushitaki ili aende mahakamani kuthibitisha hoja zake???hii ni subject to discussion.

Is CAG fooling us ?Tunahitaji mjadala!

OFISI YA CAG ni ofisi kama ofisi nyingine za umma je nani anazikagua na kuzidhibiti?
 
Ngoja tuulize. Nani anamkagua jaji??
Jaji akishatoa hukumu, nani anatoa hukumu ya kumuhukumu Jaji aliyetoa hukumu ya kwanza.

Ukishatoa majibu hapa. Utajijibu swali lako la kwanza.
Jopo la Majaji kupitia Review kama itaombwa
 
Maana yake ni wao kwa wao....nataka kujua anatumia kiasi gani mpaka anahitimisha kazi yake na kuna usafi kiasi gani katika matumizi hayo
Mwana Jangwani umepotea sana humu.
 
P Point.
Hawa officers wa CAG wanatumiaga mwanya huo kujipatia fedha. Wanajifanya wakali kumbe mwusho wake wanataka pesa.

Bado nadhani kunahitajika .mjadala juu ya riport ya CAG.
 
Hili swali huwa najiuliza sana. Kwa mfano kama hiyo hela inayopigiwa kelele 1.5 trilion kama ni uongo who makes the audit to him.
Au the assumption is that The CAG does not make mistake or in other words the CAG is God?

Or what are the underlying ussumptions for one to be the GAG or for the auditing to function.
I'm an economist i dont know the abcs of accounting works.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…