Nani kafanikiwa kununua nyumba Hamidu City kwa million 10?

Twinawe

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2016
Posts
2,431
Reaction score
5,336
Kuna huu mradi wa Kigamboni wa nyumba unaoitwa Hamidu City kiukweli umenivutia sana kutokana na uzuri wa eneo na udogo wa bei?

Mbona hizi nyumba hazinunuliki na bei ni ndogo sana tangu wazitangaze kwa bei hiyo nadhani zingeshaisha.

Kumekuwa pia na wakosoaji wakisema hilo jambo halina uhalisia kama wanavyotangaza.

Naomba mwenye ushuhuda wa mtu aliyefanikiwa kununua hizo nyumba kwa huyo bwana.

========
Your browser is not able to display this video.
 
Yani jamaa anafanya mtindo waliozoea wenzetu huko mbele unalipa kwa down payment, ila sasa yeye anachokosea ni kutangaza hiyo bei ya kuanzia tu hasemi kwamba utaendelea kulipa kidogo kidogo anajua mtajiongeza, maana zile decors tu ukiziangalia ni zaidi ya hiyo 10M na nasikia gharama halisi ya nyumba ni kama 120M
 
Nyumba milioni 10!, hiyo itakuwa ya matete na mianzi, mbavu za mbwa!
Hiyo ten ni kuanzia tu, bei yake halisi ni kama milioni, 100!
 
Acha kupotosha,
Umesikiliza tangazo lote?
Wamesema nyumba ni USD 57,000 (TZS 130,000,000), we hiyo 10mil kakuambia nani?
 
Naona wameleta style ya Nairobi
Huko kuna matajiri wamejenga nyumba za uhakika mpaka security
Hupiti Gate mpaka mwenyeji
Usalama mzuri sana huko unalala kwa amani huku
 
Ukilipa 10 unahamia au
 
Hiyo inakuwa ni ya kuanzia, baada ya hapo kunakuwa na plan ya deni. Kama hiyo plan inakaribiana na kodi yako ya mwezi, chukua. Ingawa inakuwa ni ndoa ya muda mrefu sanaaaa
 
Nawafahamu Hamidu City.

Ni wazee wa mbinu mbinu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…