Nani Kauongopea umma Mswada Katiba Mpya: Wanasheria Wanaomkosoa Lissu au Lissu?

Nani Kauongopea umma Mswada Katiba Mpya: Wanasheria Wanaomkosoa Lissu au Lissu?

Mshombsy

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2013
Posts
372
Reaction score
180
Nimekutana na habari gazeti habari leo ya wanasheria waompinga Tindu Lissu juu ya mswada wa katiba mpya nikaona niilete hapa ili wenye uelewa zaidi wa sheria wanisaidie.


“***Wanasheria hao wakaeleza kumshangaa mwanasheria mwenzao na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), kwa ushauri wake alioutangaza kwa umma, kumtaka Rais asisaini muswada huo, kwamba ushauri huo ni wa kisiasa zaidi, usio na tija kwa uongozi wala unaofuata utaratibu na sheria. Wanadai kwamba sheria isainiwe tu na rais kwamba umepitia mchakato sahihi na halali wa kikatiba.

Wamenukuliwa wakizungumza na mwandishi kwa nyakati tofauti jana, wakisema kuwa muswada huo kama ilivyo miswada mingine ya sheria, una nafasi ya kusainiwa na yakiwepo marekebisho, unarudishwa bungeni kujadiliwa na kurekebishwa.

Wakili wa kujitegemea, John Mapinduzi alisema: "Lazima muswada huo usainiwe ndipo urudishwe bungeni kwa marekebisho, Lissu ni mwanasiasa tu anapotosha umma… sasa utarudishwaje bungeni wakati ulishapita?" Alihoji Mapinduzi.

Mwanasheria mwingine wa kujitegemea, Jerome Msemwa alisema kusainiwa muswada huo ni njia sahihi na inafanyika mara nyingi (??) na kama kuna marekebisho, yanafanyika baadaye: "Wabunge kama Lissu waliamua kutoka wenyewe bungeni wakati muswada unajadiliwa… hakuna aliyewafukuza, sasa iweje leo watake usisainiwe? Haina maana leo hii kumshauri Rais kutosaini. Ushauri wa Lissu, kisheria hauna maana yoyote, hawezi kumshauri Rais leo asisaini wakati anafahamu kuwa hata baada ya kusainiwa, kuna nafasi ya kurudishwa bungeni na kujadiliwa kwa marekebisho yoyote," alisema Msemwa.

Msemwa alisema Rais asiposaini muswada huo na kuurudisha bungeni, maana yake vikao vya wabunge vilivyokaa Dodoma kujadili muswada huo, vilipoteza muda na fedha za wananchi bure. --- via HabariLeo***”

Ninavyoelewa mimi mswada ukipitishwa na bunge na kusainiwa na Rais hiyo inakuwa na ni sheria. Sasa utaratibu wa kurudisha sheria bungeni kufanyiwa marekebisho na bunge ni mrefu unaoambatana na mswada wa kuifuta hiyo sheria au kuifanyia marekebisho. Mchakato huu unakuwa ni mrefu zaidi
Sasa miswada iliopitishwa na bunge kulingana na katiba yetu ambazo rais anataka zifanyiwe marekebisho ziko mara mbili ile inayopita chini ya theluthi mbili ya wabunge, Rais anaiwekea veto yani hatosaini atairudisha bungeni kufanyiwa marekebisho.
Sasa kuna inayopita kwa zaidi ya theluthi mbili na kuua veto ya Rais, hii rais kapewa muda asiposaini na hakurudisha bungeni inakuwa sheria moja kwa moja. Ila hakiirudisha na bunge linaweza kuifanyia marekebisho na likikataa anaweza kulivunja bunge.
Sasa basi kwa hoja ya tindu lissu hataki rais asaini hiyo sheria ilirudi bungeni ili iwe rahisi kuifanyia marekebisho bila kuitaji kuanza na mswada wa kuifanyia marekebisho kwani sio sheria kamili Haikusainiwa na rais. Hao wanasheria wamekurupuka kumpinga Lissu bila kuelewa mantiki ya Lissu. Na sheria ikisainiwa tu inaanza kutumika, sasa hapa wakati wanaendelea na mchakato wa kuifanyia marekebisho kuna watu wanaweza kuitumia hasa vile vipengele vinavyolalamikiwa.
Sikatai kwamba sheria ilifuata utaratibu wa kibunge.
 
Mbali na matatizo mengine ambayo yalimfanya Lisu aseme kuwa Rais asisaini mushwada ni kutotimia kwa idadi ya wabunge waliopitisha muwada huo.Kitendo ambacho kinaufanya muswada huo uendelee kuitwa batili sijui kama hili nalo wanasheria wamelitolea ufafanuzi gani.Halafu ieleweke kuwa Lisu ni mwanasheria na ni mbunge pia kwa hiyo anaweza akawa na ufaham mkubwa kwenye mambo ya bunge kuliko mwanasheria mwingine ambae hashughuliki na mambo ya kibunge.
 
Wanasheria hao ndo wanaotumika hata ukiona majina yao yanafanana ya chama fulani , kwa mfano John MAPINDUZI. ajabu kubwa ni wao kutokutaja kama Rais akirudisha sheria hiyo ifanyiwe marekebisho Bungeni atakuwa amevunja sheria gani au kifungu gani cha katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Hofu ya CCM ni rais kutumia madaraka yake kuvunja Bunge kwani kwa hali ya hewa ya kisiasa ilivyo sasa nchini wanaweza wabunge wa CCM zaidi ya 90% kupigwa chini kama si asilimia mia kabisa. Hii inatokana na wao kutokuwa tayari kuifanyia marekebisho makubwa na yanayolalamikiwa na upinzani.
 
Hao wanasheria wa ccm nao ni wanasheria?Mbona wanashindwa kesi kila mara wanaposimama mahakamani na Lisu?
Hata ile sheria ya tozo ya line za simu ilifuata taratibu zote za kisheria hadi ilipopitishwa na bunge.Lakini je,hiyo ni sheria safi?
Huo mswada mnaosema ulifuata taratibu zote za kisheria na kupitishwa na bunge,ulijadiliwa lini? mimi niliona wabunge wa ccm wakiwajadili wabunge wa upinzani badala ya mswada.Huku ndiyo kujadiliwa kwa mswada?
Kumbukeni wabunge wa ccm ni sawa na makruta jeshini.Wenyewe ni ndiyooo afande.
Watanzania hapa tunajadili mustakabali wa Taifa kwa zaidi ya miaka 50 ijayo,hili jambo litazamwe kwa kina,Rais kikwete,Taifa linakuangalia na dunia inakuangalia pia.Mbinguni kunakuangalia na kuzimu pia.Ukicheza karata vibaya itakula kwako na vizazi vyako.Utakumbukwa kwa kudharauliwa hata na watoto ambao bado hawajazaliwa leo.
 
Tatizo la wanasheria wa CCM na baadhi ya wale wa serikali wameamua kwa makusudi kuweka taaluma mfukoni na kuwa wanasiasa.
 
mie nauhakika hapo Mh: Lissu ana pointi muhimu na siku akifumuka kuna watu watadhalilika mno...
 
Wengi wa hawa wanaojiita wanasheria ukiangalia profile zao hazina hata hadhi ya wao kuitwa wanasheria.
They are weak, incompetent and its all because hata hui uanasheria wameupata kisiasa na badala ya kuzungumza kama wanasheria wanazungumza kama wanaccm.
 
Mshombsy Mapinduzi na Msemwa wamesoma Ibara ya 97 ya Katiba kweli?????
 
Last edited by a moderator:
Wanaweza wakawa wameisoma ibara 97 ila uelewa wao ukawa mdogo
 
Tundu lissu ndiye mwanasheria bora kabisa kupata kutokea east and central africa .
 
Mara zote ndivyo wanavyoishauri serikali na CCM kufungua kesi za kijinga ijnga alafu wanabwagwa na wenye "magorofa" timamu kama akina TL!
 
Nipe kinana ya baridi, nimechoka safari ya kwenda kilimanjaro kuchek castle ikicheza.
 
Kwa bahati mbaya wanasheria waliohojiwa na HabariLeo walizungumza kisiasa zaidi kuliko kisheria. Katiba inaruhusu Rais kurejesha Mswada Bungeni bila kusainiwa kwa maelekezo. Na hii ndiyo njia sahihi na rahisi kufanya kwa Mswada ambao inaonekana una matatizo hata kabla haujawa sheria. Akishasaini inakuwa sheria na nafasi ya marekebisho inaweza hata isiwepo. Ukweli ni kuwa akishasaini Hana nguvu tena za kuurejesha Bungeni Kama Rais, Bali inabidi mkondo wa kawaida wa kubadilisha Sheria.

Rais kusaini Mswada wenye utata (ambao anajua ikiwa sheria hautatekelezeka au utaleta mtenganisho kwa jamii) kisha aurejeshe bungeni kurekebishwa, ni kitendo cha kisiasa ili kuridhidha wabunge wa upande wake.
 
Nimekutana na habari gazeti habari leo ya wanasheria waompinga Tindu Lissu juu ya mswada wa katiba mpya nikaona niilete hapa ili wenye uelewa zaidi wa sheria wanisaidie.


“***Wanasheria hao wakaeleza kumshangaa mwanasheria mwenzao na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), kwa ushauri wake alioutangaza kwa umma, kumtaka Rais asisaini muswada huo, kwamba ushauri huo ni wa kisiasa zaidi, usio na tija kwa uongozi wala unaofuata utaratibu na sheria. Wanadai kwamba sheria isainiwe tu na rais kwamba umepitia mchakato sahihi na halali wa kikatiba.

Wamenukuliwa wakizungumza na mwandishi kwa nyakati tofauti jana, wakisema kuwa muswada huo kama ilivyo miswada mingine ya sheria, una nafasi ya kusainiwa na yakiwepo marekebisho, unarudishwa bungeni kujadiliwa na kurekebishwa.

Wakili wa kujitegemea, John Mapinduzi alisema: "Lazima muswada huo usainiwe ndipo urudishwe bungeni kwa marekebisho, Lissu ni mwanasiasa tu anapotosha umma… sasa utarudishwaje bungeni wakati ulishapita?" Alihoji Mapinduzi.

Mwanasheria mwingine wa kujitegemea, Jerome Msemwa alisema kusainiwa muswada huo ni njia sahihi na inafanyika mara nyingi (??) na kama kuna marekebisho, yanafanyika baadaye: "Wabunge kama Lissu waliamua kutoka wenyewe bungeni wakati muswada unajadiliwa… hakuna aliyewafukuza, sasa iweje leo watake usisainiwe? Haina maana leo hii kumshauri Rais kutosaini. Ushauri wa Lissu, kisheria hauna maana yoyote, hawezi kumshauri Rais leo asisaini wakati anafahamu kuwa hata baada ya kusainiwa, kuna nafasi ya kurudishwa bungeni na kujadiliwa kwa marekebisho yoyote," alisema Msemwa.

Msemwa alisema Rais asiposaini muswada huo na kuurudisha bungeni, maana yake vikao vya wabunge vilivyokaa Dodoma kujadili muswada huo, vilipoteza muda na fedha za wananchi bure. --- via HabariLeo***”

.

Haya ni matatizo ya wanasheria wenye uanasiasa na kulinda matumbo yao kupitia siasa.Kwa akili ya kawaida tu hata Raisi akisaini Muswada haibadilishi hiyo hoja kupitisha Makangaja yaani vifungu vibofu na hatari kwa mustakabali wa Rasimu ya katiba na kwamba wale jamaa wa kijani walikaa chini kujadili na kupitisha utumbo na kwa maana hiyo wamekula posho /Kodi zetu bure na watakula tena bure kwa kuuwepo wao kujadili walichoshindwa kukijadili awali, wacha wenzao wawasaidie kwa manufaa ya Nchi yetu na Raisi asiwe sehemu ya Utumbo kwa kusainishwa Utumbo

Wanaukata ushauri wa Lissu na waupinzani kwa Ujumla lakini kiuhalisia Raisi akisaini na kurudisha Mswada Bungeni mwenye akili atakuwa amepata jibu kuhusu aina ya Raisi na Wabunge wa CCM!


 
Mshahara wa Mbunge ni zaidi ya M.11 kwa Mwezi, wa mawaziri ni zaidi ya M.15 kwa mwezi na mshahara wa wakili ni M 1.2-3 unategemea hakuna wakili au mwanasheria ambaye ajakomba apate japo Udunge wa kuteuliwa?
 
Nimekutana na habari gazeti habari leo ya wanasheria waompinga Tindu Lissu juu ya mswada wa katiba mpya nikaona niilete hapa ili wenye uelewa zaidi wa sheria wanisaidie.


"***Wanasheria hao wakaeleza kumshangaa mwanasheria mwenzao na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), kwa ushauri wake alioutangaza kwa umma, kumtaka Rais asisaini muswada huo, kwamba ushauri huo ni wa kisiasa zaidi, usio na tija kwa uongozi wala unaofuata utaratibu na sheria. Wanadai kwamba sheria isainiwe tu na rais kwamba umepitia mchakato sahihi na halali wa kikatiba.

Wamenukuliwa wakizungumza na mwandishi kwa nyakati tofauti jana, wakisema kuwa muswada huo kama ilivyo miswada mingine ya sheria, una nafasi ya kusainiwa na yakiwepo marekebisho, unarudishwa bungeni kujadiliwa na kurekebishwa.

Wakili wa kujitegemea, John Mapinduzi alisema: "Lazima muswada huo usainiwe ndipo urudishwe bungeni kwa marekebisho, Lissu ni mwanasiasa tu anapotosha umma… sasa utarudishwaje bungeni wakati ulishapita?" Alihoji Mapinduzi.

Mwanasheria mwingine wa kujitegemea, Jerome Msemwa alisema kusainiwa muswada huo ni njia sahihi na inafanyika mara nyingi (??) na kama kuna marekebisho, yanafanyika baadaye: "Wabunge kama Lissu waliamua kutoka wenyewe bungeni wakati muswada unajadiliwa… hakuna aliyewafukuza, sasa iweje leo watake usisainiwe? Haina maana leo hii kumshauri Rais kutosaini. Ushauri wa Lissu, kisheria hauna maana yoyote, hawezi kumshauri Rais leo asisaini wakati anafahamu kuwa hata baada ya kusainiwa, kuna nafasi ya kurudishwa bungeni na kujadiliwa kwa marekebisho yoyote," alisema Msemwa.

Msemwa alisema Rais asiposaini muswada huo na kuurudisha bungeni, maana yake vikao vya wabunge vilivyokaa Dodoma kujadili muswada huo, vilipoteza muda na fedha za wananchi bure. --- via HabariLeo***"

Ninavyoelewa mimi mswada ukipitishwa na bunge na kusainiwa na Rais hiyo inakuwa na ni sheria. Sasa utaratibu wa kurudisha sheria bungeni kufanyiwa marekebisho na bunge ni mrefu unaoambatana na mswada wa kuifuta hiyo sheria au kuifanyia marekebisho. Mchakato huu unakuwa ni mrefu zaidi
Sasa miswada iliopitishwa na bunge kulingana na katiba yetu ambazo rais anataka zifanyiwe marekebisho ziko mara mbili ile inayopita chini ya theluthi mbili ya wabunge, Rais anaiwekea veto yani hatosaini atairudisha bungeni kufanyiwa marekebisho.
Sasa kuna inayopita kwa zaidi ya theluthi mbili na kuua veto ya Rais, hii rais kapewa muda asiposaini na hakurudisha bungeni inakuwa sheria moja kwa moja. Ila hakiirudisha na bunge linaweza kuifanyia marekebisho na likikataa anaweza kulivunja bunge.
Sasa basi kwa hoja ya tindu lissu hataki rais asaini hiyo sheria ilirudi bungeni ili iwe rahisi kuifanyia marekebisho bila kuitaji kuanza na mswada wa kuifanyia marekebisho kwani sio sheria kamili Haikusainiwa na rais. Hao wanasheria wamekurupuka kumpinga Lissu bila kuelewa mantiki ya Lissu. Na sheria ikisainiwa tu inaanza kutumika, sasa hapa wakati wanaendelea na mchakato wa kuifanyia marekebisho kuna watu wanaweza kuitumia hasa vile vipengele vinavyolalamikiwa.
Sikatai kwamba sheria ilifuata utaratibu wa kibunge.

Mkuu Habari Leo na hao wanasheria ni maccm. Wala usingae
 
Conflict of interest, huyo Msemwa (nadhani ana ofisi pale Maarifa House) aliwahi kugombea Ubunge kupitia ccm jimbo 1 la Njombe, huyo Mapinduzi simfahamu, kingine ni hiki, hivi Gazeti la Habari leo mmiliki wake ni nani? Je katika mazingira hayo, mnategemea Wanasheria hao na gazeti hilo wa-comment vipi?
 
Hawa ndio wanasheria wa CCM ambao kila siku huyu huyu Lisu anawagalagaza Mahakamani katika kesi mbali mbali halafu leo hii wanajifanya kumkosoa. wanatakiwa watambue kamwe sikio halizidi kichwa.
 
Back
Top Bottom