Nani wa kuzipiga vita hizi imani potofu za kishirikina?

Nani wa kuzipiga vita hizi imani potofu za kishirikina?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Nchi hii tusioamini hayo mambo ya kichawi twaweza tusifike hata watu 100!

Humu JF yenyewe tu sidhani tunafika hata watu 6!

Wengine wote waliobaki ni watu wenye kuamini hayo mambo, ambayo kiuhalisia hayapo.

Uchawi haupo. Ni fiksi tu. Ni uongo ulio mrahisi kuugundua.

Kitendo cha binti mrembo mwenye ulemavu wa ngozi kunyakuliwa na watu halafu wakaenda kumuua na kumnyofoa baadhi ya viungo vyake vya mwili, kimeumiza watu wengi sana.

Hakuna sababu ingine ambayo inaweza kuwa ndo sababu ya kumfanyia unyama huo zaidi ya mambo ya kishirikina.

Hii si mara ya kwanza kwa mtu mwenye ulemavu wa ngozi kukutwa na dhahma ya namna hiyo.

Tanzania matendo hayo kwa hao watu yamekuwa ni ya kawaida [licha ya kwamba hayakubaliki hata kidogo].

Hivyo, hili tukio la binti mrembo si la kwanza na halitokuwa la mwisho kutokea.

Na pengine yapo matukio mengine kama hayo ambayo hayapati tu uenezi.

Naunga mkono wahusika wote wa matukio kama hayo kuadhibiwa kwa kiwango cha juu kabisa kinachoruhusiwa kisheria.

Na ingekuwa ni juu yangu kuwaadhibu wakosaji, baada kuthibitisha pasipo na shaka kuwa wanahusika moja kwa moja, sheria ningeiweka kando na kuwapa adhabu wanayoistahili!

Lakini kwenye jamii ambayo imani za kishirikina zina mizizi mirefu, ukiondoa sisi wachache ambao hatuamini kabisa hayo mambo, ni nani wa kuzikemea hizo imani potofu na kutoa elimu ya kuufuta huo ujinga?

Manake watu ambao mtu ungedhani kuwa labda ndo wanaweza kuongoza kutoa elimu na kuufuta huo ujinga, ndo wanaongoza kwenye kuziamini hizo imani potofu.

Bila kuondokana na hizo imani, matukio ya mauaji ya albino yataendelea kutokea.

Rais, ambaye ana bully pulpit ya urais, wala humsikii akiongoza kuelimisha watu kwamba uchawi au hizo imani za kichawi, ni fiksi tu.

Viongozi walio chini yake nao hamna kitu.

Hayo yote ni ishara ya kwamba hata wao wanayaamini hayo mambo licha ya fursa za kielimu na za kiufunuo walizo nazo.

Biła ya kuachana na hizo imani, hayo matukio ya namna hiyo yataendelea kutokea.

Kifo cha binti kimenisikitisha sana. Natamani ningekuwepo wakati wameenda kumnyakua maana nina uhakika binti angelikuwa yu hai leo hii.

Kitendo kama hicho hakiwezi kutokea mbele yangu halafu pasiwe na consequences kwa hao wahalifu.

I hate the emfers who took her life with passion.

I wish I would……

Pia soma:
- Update: Mwili wa Mtoto Albino (Asimwe) wakutwa hauna baadhi ya viungo

- Kagera: Kisa cha Mtoto mwenye Ualbino kudaiwa kuibiwa, RPC Makungu asema tayari wameanza uchungu

- Kufuta mauaji ya albino, ni kutokomeza kabisa Waganga wapiga ramli
 
Nchi hii tusioamini hayo mambo ya kichawi twaweza tusifike hata watu 100!

Humu JF yenyewe tu sidhani tunafika hata watu 6!

Wengine wote waliobaki ni watu wenye kuamini hayo mambo, ambayo kiuhalisia hayapo.

Uchawi haupo. Ni fiksi tu. Ni uongo ulio mrahisi kuugundua...
Halafu limetokea kipindi uchaguzi unakaribia
 
Kutoamini uchawi, hakumaanishi kuwa haupo. Uchawi upo. Misahafu imeutaja na hata Sheria za dola zipo zinazohusu uchawi.

Back to the crux of the message, ukatili uliofanywa na Hawa watu ni wa kulaaniwa ni watu Wote. Embu emagine yule Binti alilia kwa uchungu wa kiasi gani wakati akikatwa viungo vyake.

Ningependa wakitiwa hatiani, adhabu ya kifo dhidi Yao itekelezwe this time. PERIOD!
 
Kutoamini uchawi, hakumaanishi kuwa haupo. Uchawi upo. Misahafu imeutaja na hata Sheria za dola zipo zinazohusu uchawi.

Back to the crux of the message, ukatili uliofanywa na Hawa watu ni wa kulaaniwa ni watu Wote. Embu emagine yule Binti alilia kwa uchungu wa kiasi gani wakati akikatwa viungo vyake.

Ningependa wakitiwa hatiani, adhabu ya kifo dhidi Yao itekelezwe this time. PERIOD!
Ingefaa na wao wanyofolewe viungo hadharani kama vile wajerumani walivyokua wananyonga watu hadharani
 
Kuna utaratibu hapa Tanzania wa polisi kutochukuwa hatua yoyote inapopelekwa taarifa ya mtoto kupotea mpaka yapite masaa 48. Nadhani kuna haja ya utaratibu huu kuangaliwa upya.
 
Kutoamini uchawi, hakumaanishi kuwa haupo. Uchawi upo. Misahafu imeutaja na hata Sheria za dola zipo zinazohusu uchawi.

Back to the crux of the message, ukatili uliofanywa na Hawa watu ni wa kulaaniwa ni watu Wote. Embu emagine yule Binti alilia kwa uchungu wa kiasi gani wakati akikatwa viungo vyake.

Ningependa wakitiwa hatiani, adhabu ya kifo dhidi Yao itekelezwe this time. PERIOD!
Misahafu ndo habari zilezile tu. Ni riwaya za kale za watu wa mashariki ya kati huko!

Hiyo misahafu inamzungumzia mungu, siyo?

Huyo Mungu alikuwa wapi wakati binti ananyakula hadi kuuwawa?

Uchawi haupo.
 
Inasikitisha sana mkuu binadamu skuizi wamekuwa kama wanyama
 
Misahafu ndo habari zilezile tu. Ni riwaya za kale za watu wa mashariki ya kati huko!

Hiyo misahafu inamzungumzia mungu, siyo?

Huyo Mungu alikuwa wapi wakati binti ananyakula hadi kuuwawa?

Uchawi haupo.
Mambo ya ushirikina kila mtu abakie na anchoamini. Wewe kama umekulia ng’ambo huezi elewa mambo ya uswazi, mijin na vijijini.

Ila wote tunakemea vitendo viovu hasa dhidi ya binadamu.
 
Kuukataa ukweli kuhusu uwepo wa tatizo kama ambavyo una jaribu kufanya mtoa mada, ndio kutafanya tatizo liongezeke zaidi..

Unacho kifanya mtoa mada ni sawa na muathirika ambae hataki kukubali kwamba ameathrika halafu wakati huo huo anataka kupata mwarobaini wa tatizo lake.

Kubali kwanza kuwa tatizo lipo ndio utaweza kupata suluhisho la tatizo.
 
Kuukataa ukweli kuhusu uwepo tatizo kama ambavyo unavyo jaribu kufanya mtoa mada, ndio kutafanya tatizo liongezeke zaidi..

Unacho kifanya mtoa mada ni sawa na muathirika ambae hataki kukubali kwamba ameathrika halafu wakati huo huo anataka kupata mwarobaini wa tatizo lake.

Kubali kwanza kuwa tatizo lipo ndio utaweza kupata suluhisho la tatizo.
Nimeukataa ukweli upi? Kwamba uchawi haupo?
 
Mambo ya ushirikina kila mtu abakie na anchoamini. Wewe kama umekulia ng’ambo huezi elewa mambo ya uswazi, mijin na vijijini.

Ila wote tunakemea vitendo viovu hasa dhidi ya binadamu.
Endeleeni kuamini hivyo na watu wataendelea kuuwawa kipumbavu pumbavu namna hiyo.
 
Back
Top Bottom