Nani Zaidi: Member Wakongwe Vs Member Wachanga.

"Huenda hao wapya ni zao la wakongwe", baadhi ya ID's ni watu walewale tu, wengine waliharibu wakaamua kuja kivingine, wengine walichoka zile identity zao wakaamua kubadili na wengine walisahau hata password zao wakabadili usernames.
 
Member wa zamani walikuwa viazi pathetic kabisa

Sasa hivi wamekumbwa na radi ya life ya Magufuli wote wamepoteana
 
Wote sawa tu kunabaadhi ya members wazamani wanaandika hovyo kabisa content zero pia kunabaadhi ya members wasasa wanaandika makaliozi ko wote sawa tu sema wakongwe tuwape heshima Zao waendelee kudumu japo wanakufa kimantiki kwa kasi ya jiwe akidili na uopoaji kule ukara
 
Mm niko nje ya mada ila naona heri mtu awe hivii.. na mm ni mgeni ila naona aliye bora humu c wa zamani au wa sasa bali ni yule anayejiamin kutumia jina lake ktk jf.. sio manick names kibao.. kwa nn ujifiche wakati unajiamin humu tumia jina lako kuchangia mada na kuleta changamoto humu jf.. najua nitawakamata wengi tu 99% ya members wa humu wanajiita majina ya ajabu na wanajiona wao ni wakongwe... mababu zetu na mabibi zetu walikuwa hawana majina ya namna hiyo..member anayejiamin na mjanja humu anayetumia jina lake kamilii... haijalishi avatar yake. Bali real name huyo ndo mjanja wa jf..😁😁😁😁.
 

Wakongwe ndo mambo yote kwanza hata mada zao zimeenda shule ni tofauti na wapya kila kukicha ni kuomba msaada tuu mara eti nakawia kufika kileleni.. mara nashindwa kumtongoza mara nifanyeje nimtoe bikra yake yaani utoto mwingi tena ukiona uzi wa wakongwe hakunabhata mpya hata mmoja anacoment ya maana zaidi ya kuponda
 
Mimi ni new member since 2017 lakin hoja sio new member au old member lakin hoja ni wanao ihalibu JF ni watoto wadogo yaan kuna mtu anaweza kuwa new member lakin ege yake 35+ so mtu huyu mada zake zitakuwa zakikubwa tu awezi andika upupu even a little bit lakin -25 awa member wamejaa utoto mtupu nyuzi mbovo akuna mfano
 
Member wote wanamchango wao muhimu sana....Mimi naona wote wapo poa maana wachanga wanachangamshano group then wapo social kinoma noma.....

Alaf mada pia za member wachanga muda mwingine zinaondoa stress,presha,magonjwa ya ngozi, kansa,pamoja na kutibu magojwa ya ngono
 
hahaa hata Mkopo unaweza kuziombea
 
"Huenda hao wapya ni zao la wakongwe", baadhi ya ID's ni watu walewale tu, wengine waliharibu wakaamua kuja kivingine, wengine walichoka zile identity zao wakaamua kubadili na wengine walisahau hata password zao wakabadili usernames.
Mkuu hii comments yako ya pili sasa" naona unaliongelea hili " huwenda ikawa kuna ukweli ndani yake
 
Mimi niseme tu bila kumung'unya ".... nikweli JF ya sasa ina mapungufu makubwa sana", haswaa kwenye mada ambazo ni fikirishi'.... JF imepoteza watu Makini wenye michango tija" ambayo inaweza kukufanya uvute kiti uanze kuifuatilia mpaka usahau hata kula"....


Mfano mdogo(mzuri), siku hizi majukwaa yanayoiendesha JF ni chit chat na MMU " wakati zamani haikuwa hivyo"...., ilikuwa nilazima kwanza upitie kwenye majukwaa haya"... JUKWAA LA SIASA. JUKWAA LA INTELLIGENCE " JUKWAA LA BIASHARA".. NA INTERNATIONAL FORUM".. kisha baadae ndio unakuja kutuliza akili kwa kutembelea hayo majukwaa mengine"..., na hayo majukwaa mengine ulikuwa ukienda unakutana na mada moto moto"...,JF imepoteza watu Kama Deception mnepha lara 1 newton Einstein "... na wengine wengi ambao kichwani walikuwa na material adimu kabisa " yakukufanya ujione kuwa wewe ni kilaza unayepaswa kujifunza toka kwao"....,

huu ni wakati sahihi sasa" wasisi kujitathmini upya ili tuone tunatakiwa kufanya nini ili kuirejesha heshima ya JF mahala pake"..... zamani hata mods walikuwa wanaanzisha thread au wanachangia mada', kwa sababu walikuwa wanapatwa na ushawishi unaosukumwa na ubora wa topic zilizokuwa zinaletwa" Jf lakini siku hizi hauwezi kukutana na hiyo kitu".... nachelea kusema hata GENTAMYCINE yule wa miaka miwili nyuma sio huyu wa leo (hahaaa naomba unisamehe wewe mtutsi) ....


Japo kuwa ukweli huwa mchungu" lakini tuwe na desturi ya kuumeza tu" maana ndio tiba ya kujitathmini

nawasilisha
 
Sie wapya ndo noma sana.. hao wahenga tupa kuleee..
 
member wa kongwe wananzia mwka Gani na member wapya wnaanaanzia mwaka upi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…