Naomba kuelekezwa jinsi ya kutengeneza visheti

tian

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2007
Posts
1,770
Reaction score
537
Kwa mwenye uzoefu tafadhali anieleweshe.
 
E nimeandika mlolongo mrefu halafu umeruka aghhhhh siku nyengine tian
 
Last edited by a moderator:
Yaani tangu mda huo naandika halafu hata sikuona post imerukia wap lol...uchungu
 
tian Nakuelekeza tu bila vipimo. Vipimo hadi siku nikipika.

Changanya unga + chumvi + sukari kidogo km kijiko kimoja + iliki + samli iliyoyayushwa / mafuta+baking powder kidogo
Changanya vizuri fikicha usiwe na madonge Weka tui zuri au maziwa kwenye mchanganyiko taratibu huku unakanda hadi upate donge moja (lisiwe gumu na wala laini kupitiliza ) liweke pembeni km robo saa. Chukua unga ukate madonge halaf Tengeza minyororo mirefurefu ukate kwenye kibao ( ukipenda kutengeza shape tofaut unaweza kuchukua chujio au grater baada ya kukata uvigandamizie kidogo )
Teleka karai la mafuta uvichome hadi viwe golden brown. Viwache vipoe.
Tengeneza shira kutumia sukari + maji + iliki / vanilla Chemsha hadi iwive, ili kujua km imewiva vizuri ukiigusa utaina inanyamata au ina uzito flani hivi Au njia nyengine chukua kikomba weka maji kidogo halafu tonyeza ile shira ndani ya kikomba utakuta lile tone limeenda moja kwa moja kukaa chini ya kikombe.
mimina vile visheti vyako vilivyopoa huku ukivipetapeta.
Km shira iliiva vizuri utaona vimekauka mara moja .

Nb. Watu wanaweka had maziwa ya unga /castard etc farkhina Angel Nylon kwa utaalam zaidi
Cc Honey Faith mambo yako
 
Last edited by a moderator:
Fakhrina hujambo mamii..natamani kupika hivi visheti..naomba vipimo nijimwage Leo Ramadhan 21..hivi naenda nunua hiyo castard
 
Hv kwa mtu anaetaka kuuza atapata faida kweli km mahitaji yake yanaonekana kuwa ya gharama sn??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…