Naomba kufahamishwa maana za maneno haya

Naomba kufahamishwa maana za maneno haya

Alejandroz

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2017
Posts
329
Reaction score
413
Muishi milele wadau wa jf

Naomba kufahamishwa maana za maneno haya kama yanavyotumika katika dini yakiislamu;
- Juzuu

- Kuran

- Msaafu

- Ulamaa

Karibuni
 
Salaam ndugu,

Najaribu kukueleza kwa ufupi hapa:

Juzuu maana yake halisi ni "sehemu") ni moja ya sehemu thelathini za urefu tofauti ambapo Quran imegawanywa.

Quran ni maandiko makuu ya dini ya Kiislamu, yanayoaminiwa na Waislamu kuwa ni ufunuo kutoka kwa Mungu. Quran imepangwa katika sura 114 na Juzuu 30

ULAMAA: Ni wajuzi wa uislamu, ambao wamehusishwa na uchambuzi wa hukmu za kiislamu, na wakaasisi kwa ajili kudhibiti misingi ya halali na haram, na wao katika ardhi nafasi yao ni kama nyota katika mbingu, kupitia wao huongoka waliopotea katika viza, na haja ya watu kwao ni zaidi ya haja yao kwenye chakula na kinywaji.

Msahafu, kitabu kitakatifu cha kislamu. Kimeundwa na Juzuu 30 na sura 114
 
Salaam ndugu,

Najaribu kukueleza kwa ufupi hapa:

Juzuu maana yake halisi ni "sehemu") ni moja ya sehemu thelathini za urefu tofauti ambapo Quran imegawanywa.

Quran ni maandiko makuu ya dini ya Kiislamu, yanayoaminiwa na Waislamu kuwa ni ufunuo kutoka kwa Mungu. Quran imepangwa katika sura 114 na Juzuu 30

ULAMAA: Ni wajuzi wa uislamu, ambao wamehusishwa na uchambuzi wa hukmu za kiislamu, na wakaasisi kwa ajili kudhibiti misingi ya halali na haram, na wao katika ardhi nafasi yao ni kama nyota katika mbingu, kupitia wao huongoka waliopotea katika viza, na haja ya watu kwao ni zaidi ya haja yao kwenye chakula na kinywaji.

Msahafu, kitabu kitakatifu cha kislamu. Kimeundwa na Juzuu 30 na sura 114
Shukran kwa ufafanuzi mzuri ndugu
Ila bado napata ukakasi wakutofautisha Kuran na Msahafu

Nimeelewa kuwa vyote ni vitabu au maandiko matakatifu ya kiislamu yenye sura 114 na juzuu 30

Je, tofauti yake ni nini hasa?
Naomba ufafanuzi zaidi
 
Shukran kwa ufafanuzi mzuri ndugu
Ila bado napata ukakasi wakutofautisha Kuran na Msahafu

Nimeelewa kuwa vyote ni vitabu au maandiko matakatifu ya kiislamu yenye sura 114 na juzuu 30

Je, tofauti yake ni nini hasa?
Naomba ufafanuzi zaidi
Habari ndugu,

Hapo ni sawa na kusema biblia na neno.

Msahafu ni kitabu kilichohifadhi vitabu 30 Quran.

Msahafu kwa dhana yake ni kama biblia na Quran kwa dhana yake ni kama neno lililo ndani ya biblia.

Hivyo, waislam wanasoma Quran (Maneno ya Allah) yaliyohifadhiwa ndani ya Msahafu (Kitabu).
 
Habari ndugu,

Hapo ni sawa na kusema biblia na neno.

Msahafu ni kitabu kilichohifadhi vitabu 30 Quran.

Msahafu kwa dhana yake ni kama biblia na Quran kwa dhana yake ni kama neno lililo ndani ya biblia.

Hivyo, waislam wanasoma Quran (Maneno ya Allah) yaliyohifadhiwa ndani ya Msahafu (Kitabu).
Sasa nimekuelewa [emoji1431][emoji1431]
 
Back
Top Bottom