Naomba kufahamishwa, taratibu za kujitambulisha na kutoa kishika uchumba ukweni

Hongera mkuu, pambania kombe hilo ubebe mke!!

Ila kikwetu kuoa ni simple kabisa, hizo complications hazipo
 
Npo mbali na home na Wala siishi home! mzee wangu ashatangulia mbele za haki muda mrefu Sana, nlimweleza mother akaniambia hayo nifanye mwenyewe maana kimila yeye haruhusiwi!

Kuuliza sio ujinga, Nataka nijazie mambo yaende vzur!
Huna wajomba wala baba wadogo....wala kaka ..utakuwa kiumbe wa ajabu ukikosa wote hao
 
We kwenu huna wakubwa zako au Wazazi wako, Mjomba au Kaka zako wakubwa, au Kiongozi wako wa Dini.

Cheki na hao watu kwanza watakupa Muongozo sahihi kufanikisha suala lako
 
Kabila gani mkuu
 
Huna wajomba wala baba wadogo....wala kaka ..utakuwa kiumbe wa ajabu ukikosa wote hao
Mkuu kama umebarikiwa kuwa na watu wote hao mshukuru sana Mungu, sijui kuhusu huyu muhusika ila nikijiongelea mimi binafsi hao wote uliowataja mimi sina la kaka tu ambaye kiumri hatujapishana sana, sisi tumelelewa na mama nashukuru alitusomesha tukakua na sasa tunajitegemea, nilipokua mdogo na mimi nilitamani niwe na ndugu kama marafiki zangu sasa nimekua na ulimwengu umenipa ndugu wa kutosha nashirikiana nao kwenye maisha ya kila siku, hivyo usishanga kusikia mtu hana baba,mjomba wala shangazi ni kawaida tu na ninaamini wapo wengi tu kama mimi.
 
Umemissinterpret maanani yangu.... Unafikiri kaka ni wa kuzaliwa tumbo moja!!!?? Yaaani baba yako hakuwa na mdogo wa kile wala wa kiume !!? Mama yako hakuwa na mdogo wa kike wala wakiume !!??hawana watoto au ndio wale wakifanikiwa wannakimbia ndugu wakifariki watoto mnabaki yatima hata kwa ndugu mnaogopa kutembelea !!??

Yaaani ubaki moja hivi acha hizo we jamaa ndugu wapo tunawakimbiankwa umasikini wao au utajiri wetu ..ila ndugu wapo wengiiii mno tatizo mnachagua wa kuwa ndugu zenu.
 
mkuu narudia kukwambia tena kama umebarikiwa kuwa na wote hao mshukuru sana Mungu
 
Ngoja mchumba wako aje hapa atoe maelekezo ya kwao, uzuri ID yake imo humu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…