Kwanza Bima za magari zipo za aina mbili Kuna Bima kubwa (comprehensive) Na Bima Ndogo(third party), Ya kwanza ina ghrama kubwa kwa sababu hii inalinda risks zote pamoja na gari lenyewe , na ya pili ni kwa ajili ya mtu yeyote atakaye athirika kutokana na matumizi yako ya gari kama vile mtembea barabarani uliye mgonga n.k Hivyo ukikata bima hii ndogo, gari lako linakuwa halilindwi bali ni kwa ajili ya lawama zatakazotokea.
Na kuhusu gharama, hakuna kiwango kamili kabisa, ila kinatofautiana kulingana na makampuni ya Bima, Thamani ya Gari lako(sum insured), aina ya cover unayokata(kama nilivyoainisha hapo juu), Matumizi ya hili gari lako kama ni biashara au private!