Wanajanvi naomba kujuzwa kama kuna sheria inayomlazim mtu kuomba kibari ili kifanya maandamano yawe ya arusi au ya chama au unatoa taarifa tu vyombo husika kama polisi?
Ndio unatakiwa kutoa taarifa kwa maandishi polisi, ueleze unaandamana kwa sababu zipi na wao wakiona hakuna viashiria vya uvunjifu wa amani watakuruhusu na kama si shwari utazuiliwa.
Nashukuru ila bado sijajibiwa nadhani. Hiyo sheria inasemaje na ya lini maana naona wengi mnasema kuijurisha polisi lkn sijaona kuwa inakulazim uombe kibari na upuwe kibari.
Kwa upande wa kuandamana kwa vyama sheria inapatikana kwenye sheria ya vyama vingi au The Political Parties Act Cap 258 R.E. 2002) kifungu cha 11(4-8). Pia haki hiyo inapatikana kikatiba soma kifungu cha 17 uhuru wa kwenda unakotaka mradi huvunji sheria
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.