Naomba kujua kuhusu taratibu za mahakama zetu Tanzania

Naomba kujua kuhusu taratibu za mahakama zetu Tanzania

jaffari odhiambo

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2014
Posts
526
Reaction score
13
Katika mahakama ya wilaya ya Bunda -Mara kuna wafanyakazi wanaoitwa makarani. Sasa ukienda pale ili ujaziwe fomu halafu usainiwe na mh. Hakimu unaombwa hela ati hakimu hawezi kusaini bila hela. Je, huo ndio utaratibu ama ni rushwa ya kijanja janja? Naomba kueleweshwa maana sijui kama ndio utaratibu wa mahakama hizi zetu za TANZANIA ama ni utaratibu wa pale BUNDA tu ama namna gani. Mnifahamishe jamani wanajamvi wenzangu. Hela yenyewe ni sh.5000 tu ya kitanzania.
 
Hiyo ni rushwa wala hakuna kitu hapo maana mh.Hakimu hawezi kuomba sh.5000 kwa ajili kusaini. Hao ni matapeli ni rushwa.
 
Jamani kwa kawaida ukitaka kucertify unalipia wanandugu.. ni 5000 wala si rushwa. Kwa mawakili ni kuanzia 15000. Makaran hawajakosea
 
Sasa kama ni kweli na halali mbona hawatoi risiti ya hiyo hela? Bado nina wasiwasi hapo.
 
Jamani kwa kawaida ukitaka kucertify unalipia wanandugu.. ni 5000 wala si rushwa. Kwa mawakili ni kuanzia 15000. Makaran hawajakosea
Tatizo hela ina ingia mahakamani? au ofisi ndani ya mahakama?
 
Back
Top Bottom