Aliyekuwa mbunge wa Kasulu Kigoma na mwanachama wa Chadema Mh. David Kafulila amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar Paul Makonda aonyeshe vyeti vya elimu yake ili nchi iendelee na mambo mengine
Kafulila pia ameshangazwa na ukimya wa mamlaka ya uteuzi na wizara ya elimu na vyuo alivyosomea Makonda. Kwa kawaida vyuo alivyosomea Makonda vinatakiwa kuchukua hatua kupata uhakika wa ukweli wa jambo hili ili hatimaye vifute vyeti vilivyomtunuku Makonda kwa kuwa hakuwa na sifa za kudahiliwa.
David Kafulila amemtaka Makonda ajiuzuru kama hana vyeti ili hatua za kisheria zifuate