Ndugu zangu hapa nilipo hali ya sinto fahamu, jana kwenye pita pita zangu nilikutana na mama mmoja nesi "nadhani" akiwa anawapima watu "presha ya mwili" ilikuwa maeneo ya sokoni na mimi nikavitiwa nikasogea nilipopima akaniambia nina presha 94 mimi ni mwembamba urefu 172cm uzito kama 63kgs .
Hivi hapa nilipo sijielewi hili tatizo limenipataje ilaa muda ananiwekea kipimo nilishtuka kidogo sijui kilitoa majibu sio ama vipi ila sikutaka tena kuruka tena kupima kwake.
Naombeni kujua kiwango kizuri cha presha ni kipi na ushauri nifanyaje kukaliana nalo kwa sababbu bado siumwi sehmeu yeyote.