Naomba kujulishwa gharama za kuipata Coaster

Naomba kujulishwa gharama za kuipata Coaster

Weakman

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2021
Posts
995
Reaction score
1,607
Ndugu zangu humu ndani!

Mimi ni mvuja jasho mwenzenu, nipo Mtwara Masasi, namiliki Hiace mbili ambazo kwakweli naona biashara imedorora kabisa.

Kuna wakati biashara haikuwa mbaya sana, Ila coaster nyingi zimekuja kutuharibia, maana hata abiria wanapendelea kuingia kwenye coaster!

Nimekuwa na wazo niachane nazo Hiace nichukue Coaster japo hata wenye coaster wanalalamika biashara ngumu!

Naomba kujua gharama ya kuipata Coaster kutoka yard, au mikononi mwa mtu au namna yoyote ambayo inawezekana ili nijue namna ya kujipanga!

Nitashukuru kwa kupata ufahamu!
 
Hata wenye coaster/canter/fuso/town ace/kirikuu nao wanalia.nadhan biashara zimedorora kwa upana wake.
Unaeza nunua coaster ma usione mabadiliko uliyotarajia kimahesabu.
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Ndugu zangu humu ndani!

Mimi Ni mvuja jasho mwenzenu, nipo Mtwara Masasi, namiliki Hiace mbili ambazo kwakweli naona biashara imedorora kabisa!
Kuna wakati biashara haikuwa mbaya Sana, Ila coaster nyingi zimekuja kutuharibia, maana hata abiria wanapendelea kuingia kwenye coaster!

Nimekuwa na wazo niachane nazo Hiace nichukue Coaster japo hata wenye coaster wanalalamika biashara ngumu!

Naomba kujua gharama ya kuipata Coaster kutoka yard, au mikononi mwa mtu au namna yoyote ambayo inawezekana ili nijue namna ya kujipanga!

Nitashukuru kwa kupata ufahamu!
Mtu anayemiliki Hiace mbili hajui namna ya kupata Coaster? Mtu anaingia na JF?

Acha masiala ndugu
 
Back
Top Bottom