Biashara ambazo unaweza kupeleka Mafia,
1.Vyakula-maharage, mchele, Unga, mafuta ya kula.
2.Nguo za Mitumba au hata special ila ziwe na bei reasonable.
3.Kuna uvuvi kule waweza peleka net za kuvulia samaki.
Kutoka uko
1.Samaki
2.Mazao ya baharini, kaa,pweza,ngisi,kamba,kambakoche.
Mkuu una mtaji wa kiasi gani? Kama una angalau 30 mil nitafute nikupe mchongo kiroho safi. Mafia hela ipo.Wakuu,
Naomba kwa wale walio kwisha kutembelea katika visiwa hivi Mafia na Songasi, wanisaidie kujua yafuatayo:-
Ni biashara gani naweza kutoa uko kuleta apa Dar au ni biashara gani naweza kutoa Dar kupeleka uko.Najipanga kwenda kutembelea kwanza ila nimeona niulize nipate mwanga kabla sijaenda.
Natanguliza shukrani.