Naomba kujuzwa kuhusu majina yaliyotolewa na hivi vyuo

Patflax jr

Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
72
Reaction score
1
Wanajamvi naombeni msaada. Naona majina mengi yaliotolewa na hivi Vyuo ambavyo tayar vimeshatangaza majina ya waliochaguliwa, wengi ni Form Six freshers au mie nimeona vibaya?? Sasa swali ninalotaka kusaidiwa ni kuna ambae ni Inservice alieomba kupitia Equivalents/diploma ambae ameona jina lake??? Msaaada wakuu maana hapa mambo hayaendi wala hayarudi
 
yaa udsm wapo wachache ngoja uwe na subira na vyuo vingne
 
dah! Wadau mie nimewaelewa ila ukiangalia udsm wengi wao ni wale waliomaliza Form Four 2011 means f6 ni 2014 ambao ndo takriban 99% na hao wengine utakuta wamemaliza f4 kwenye 2010 au 2009 ambapo kwenye O-level result zao kuna seats zaid ya moja nikiwa na maana kuwa wemerisiti mitihani na kama ni inservice bas walau wangekuwa wamemaliza F4 kwenye miaka ya 2007 kurud nyuma ili walau tuwe na ile miaka kadhaa ya kusomea taaluma.

Hapa ndo nachanganyikiwa nahisi kwa UDSM hakuna inservice
 

Ndugu ya ni vyema umeuliza nami nilikuwa nina maswali mengi kuhusu inservice maana kwenye colum ya diploma hakuna kilicho jazwa hata ukitazama nafasi zilizotolewa kwa mfano MUCE capacity ya walioomba kupitia Diploma ni 30 kwenye orodha iliyotoka UDSM ni wanafunzi 45 tu ina maana form six walikuwa na nafasi 15 tu? jamani mnao lifahamu zaidi ili tunaomba ufafanuzi
 

Dah kaka Ud wamechukua dip ya education mmoja tu mwenye gpa 4.4 so si wenye 3.5 hadi 3.0 chuo chetu ni UDom. For sure Ud wana ubaguzi
 
Dah kaka Ud wamechukua dip ya education mmoja tu mwenye gpa 4.4 so si wenye 3.5 hadi 3.0 chuo chetu ni UDom. For sure Ud wana ubaguzi

Sio ubaguzi wacha waliofaulu vizuri wapate vyuo vizuri.........

Na wewe utapata mahali panapo kufaa......mbna bs in textile wamepata udsm kwa 4.
 
Sio ubaguzi wacha waliofaulu vizuri wapate vyuo vizuri.........

Na wewe utapata mahali panapo kufaa......mbna bs in textile wamepata udsm kwa 4.

mkuu hakuna ishu ya chuo kizuri wala chuo kibaya. ishu hapa ni kwa nini wengine watuache kama sio ubaguzi? kwanini wachukue mtu mmoja tu? ina maana tunao apply kwa diploma hatukusoma zaidi ya hawa form 6 wa BRN ambao hata mitihani yao tumesahisha na kushuhudia madudu yao?!
Hivi unajua diploma ya ualimu ina masomo mangapi? unajua mwenye gpa 3.5 amefaulu kwa kiwango gani?
Udom tutapata na tutakwenda ila ukweli unabaki pale pale ud ni wabaguzi.
 


Ndugu mwalimu ulienda marking ya mitihani ya form six?
And now umeapply kwenda kusoma degree
 

Wewe acha majungu kwani nani aliyekwambia ufeli Form6 kwenye miaka yenu? Acha vijana wabichi fresh from school wakale maziwa na asali ya UDSM wewe apply TEKU na Amazon college ndio mahali pako.
 
Wewe acha majungu kwani nani aliyekwambia ufeli Form6 kwenye miaka yenu? Acha vijana wabichi fresh from school wakale maziwa na asali ya UDSM wewe apply TEKU na Amazon college ndio mahali pako.

Mkuu wewe utakua chizi, so kwa akili yako kila mwenye diploma alifeli form 6?!
elewa wengine tulikuja huku baada kwenda chuo halafu bodi kuzingua boom so hatukupoteza muda tukakamata fursa ila sio kwamba tulifeli form 6 panua akili kijana.
 
Ndugu mwalimu ulienda marking ya mitihani ya form six?
And now umeapply kwenda kusoma degree

elewa kipi nime maanisha hapo. ni kwamba hawa vijana ambao leo wanapewa kipaumbele kwa ufaulu wao wa brn walipokua form 4 pepa zao tuli mark sisi ambao leo ud wanatubagua kwakua tu tunataka kujiunga pale kupitia diploma.
 
Mkuu wewe utakua chizi, so kwa akili yako kila mwenye diploma alifeli form 6?!
elewa wengine tulikuja huku baada kwenda chuo halafu bodi kuzingua boom so hatukupoteza muda tukakamata fursa ila sio kwamba tulifeli form 6 panua akili kijana.

Sasa tatizo mkuu una hoja nzuri lakini wewe umeiwasilisha kimajungu zaidi thus why nikakujibu kimajungu all in all amani mkuu.
 
Sasa tatizo mkuu una hoja nzuri lakini wewe umeiwasilisha kimajungu zaidi thus why nikakujibu kimajungu all in all amani mkuu.

Naamini sasa umenielewa. hata guide book ud walitoa entry requirements kwa wenye diploma ambazo watu wamekidhi ndio tuka apply ualimu wametaka credit,upper second or average of B.
Sasa credit ni gpa 3.5 mpaka 4.4

capasity ud zilikua 100maajabu yao sasa wechukua mmoja tu wa gpa 4.4 i.e acha hii gpa 3.5 ambayo crdt inaanzia wapo hadi 3.8 wameachwa wakati capacity 10 waliyoweka wenyewe haikujaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…