Naomba kujuzwa: Kwanini hukumu katika mahakama zinatolewa kwa Kiingereza tu?

Naomba kujuzwa: Kwanini hukumu katika mahakama zinatolewa kwa Kiingereza tu?

Fisi wa Dar

Member
Joined
Apr 2, 2018
Posts
69
Reaction score
52
Nimejaribu kudadisi wanaonijibu wanasema hawajui, hebu wenye weledi na vitu hivi mnisaidie!
 
Kizungu hiki.
We acha tu!
Mbele ya pilato nikahukumiwa kwa kiingereza. Sikusikia vizuri, nikahisi kama amesema nimehukumiwa jela mwaka mmoja. Nusu nidondoke na kuzimia. Kumuuliza msaidizi wake akasema kuwa nimehukumiwa kwa kuwekwa chini ya uangalizi mwaka mmoja na sitakiwi kutenda kosa kama lile.
Hii ilitokea baada ya dereva wangu kusababisha ajali ya gari na mie sikuwa nimezingatia kama ana nyaraka muhimu ikiwepo leseni inayoendana na daraja la gari alilokuwa analiendesha.
 
Kizungu hiki.
We acha tu!
Mbele ya pilato nikahukumiwa kwa kiingereza. Sikusikia vizuri, nikahisi kama amesema nimehukumiwa jela mwaka mmoja. Nusu nidondoke na kuzimia. Kumuuliza msaidizi wake akasema kuwa nimehukumiwa kwa kuwekwa chini ya uangalizi mwaka mmoja na sitakiwi kutenda kosa kama lile.
Hii ilitokea baada ya dereva wangu kusababisha ajali ya gari na mie sikuwa nimezingatia kama ana nyaraka muhimu ikiwepo leseni inayoendana na daraja la gari alilokuwa analiendesha.
Pole sana mkuu. Ilikuwa mahakama ya ngazi gani?
 
Zinaandikwa kwa sababu ya 'urahisi wa tafsiri'. Ukisoma nyaraka za kisheria kwa lugha ya kiswahili zinaleta shida katika tafsiri (interpretation). Kuondoa ambiguity kiingereza kinatumika.
 
Back
Top Bottom