Naomba kujuzwa namna bora ya kupika ugali wa dona

Naomba kujuzwa namna bora ya kupika ugali wa dona

Joined
Jan 28, 2022
Posts
42
Reaction score
43
Mimi ni mpenzi wa ugali dona mix ya Mahindi, ngano, mtama/ulezi mweupe. Ningependa kujua namna bora ya kuupika ukakujulisha kuwa umeiva.

Hata kama kuna mix iliyo bora zaidi, nijulishwe.

1654257639825.png

Picha kutoka Maktaba
 
Sijawahi ona tofauti muhimu na kuhakikisha uji unachemka vyema kabla ya kuanza kusonga, na ukishasonga bas hakikisha unakaa jikon s chin ya walau dk 4/2 huku ukiendelea kusonga na kuuacha.

Sasa ndyo ugali tuupikao; mahind ya njano yasiyokobolewa, ngano, na makopa ya ndzi mchanganyiko huu ndio utupao ugali tuulao kila leo. Hatujawah songa ugali ukawa mbichi, tunazngatia hayo niliyokujulisha hapo juu.
 
Ugali wa dona unakuwa mzuri ukiuchanganya na unga wa muhogo(udaga)... Usipike mgumu na wala usiwe mlaini sana,kooni unapita bila vurugu pia ni lishe moja wapo yenye kupendeza zaidi!.

Unaendana na mboga takribani zote iwe nyama fresh,iwe maharage bomba,mboga za majani ukikuta imewekwa na karanga unaweza jilamba kisogo! Samaki ndo hadi chozi linataka kunitoka kabisa!.

Faida nyengine ya dona halikai sana tumboni, Wala sembe wanatabu sana haswa ukikuta mtu hanywagi na maji kinyesi kinakuwa kigumu ndio maana wanaugua na bawasiri!, hawana uhakika wa kupata kila siku choo! Hiki ni kitu mbovu mbaya kwa afya ya mwanadamu aliekamili!.

Mwisho niwahase watanzania wenzangu tupunguze Sana matumizi ya vyakula vya wanga,heri kwa ambae anafanya kazi za nguvu wale wa kukaa tu mtaota vitambi Kama mnakulaga rambirambi..!
 
Back
Top Bottom