Naomba niweke hili kwa lugha mbili pale inapobidi kutokupoteza maana. Hilo la permit ya siku 90 ni sawa inaitwa temporary importation na lazima ulipie. Free entry ni week mbili kama sikosei unataka kuja na gari yako Tanzania yenye usajili wa Burundi. Kama ni zaidi ya muda wa free entry utaweza kulipia kwa mwezinau miezi mitatu sema kuna kikomo na kuongeza muda itabidi uende ofisi za TRA.
Kama unataka kuleta gari lenye usajili wa Burundi kuja Tanzania kwa maana kufanya usajili inabidi kufuata karibu processes zote kama vile uliagiza gari kutoka Japan, UK n.k. sema kuna urahisi kidogo kwa sababu gari tayari liko kwenye Jumuiya ya EAC na Customs process hata details za gari zipo .
1. De-registration ya gari Burundi, tumia agent anajua hizo process kama ni Bujumbura kwani border taasisi za serikali kama vile wakala wa usafiri wanaweza kuwa hawapo.
Peleka original card wakala wa usafiri sijui huko wanaitwaje kwa ajili ya kufuta usajili hapa uwe tayari na information kama vile kodi Tanzania itakuwa kiasi gani na gharama za agents, insurance, Interpol certificate usije kubadilisha mawazo na gari imeshafutiwa usajili.
2. Uwe na barua na viambatanisho hiyo gari ni yako na documents kama passport visa au barua ya muajiri kama ulikuwa umeajiriwa (unaweza kupata exemption ya kodi kama ulikuwa unafanya kazi Burundi kwa zaidi ya mwaka na barua ya mkataba kuisha angalia
www.tra.go.tz maelezo yapo vizuri)
3. Utapeleka gari Interpol na customs ya Bujumbura au mkoa wowote wenye hizo huduma ila mara nyingi makao makuu kwa ajili ya police clearance na utapewa certificate kama gari haiko kwenye list ya magari yaliyoibiwa au kufanya makosa.
4. Utatakiwa kufanya inspection ya gari na TBS kama kuna wakala huko ila unaweza kufanya border.
5. Utakuwa umeshachagua customs agent wa kufanya hizo process upande wa Burundi na Tanzania na uwe na copy ta TIN ya Tanzania.
6. Agent wa Burundi chini ya Single Customs Territory ya EAC ataingiza hizo documents online na maofisa wa customs wa TRA na Burundi watakagua gari kama ni Bujumbura au border na kuweka report kwenye mtandao
7. TRA makao makuu Dar watakagua hizo documents na kupitisha uingizaji wa gari.
8. Malipo kama ushuru, tozo, usajili wa gari, TBS, yatalipwa kabla ya kibali cha kuingiza gari kupitishwa wakati gari lipo Burundi.
9. Gari litapita kutumia border husika mfano Manyovu, Kobero baada ya TRA kutoa exit note na itatumia temporary plates..mara nyingine unarudisha original plate number unachora kibao kingine kinaanza na EX..plate number iliyofutwa.
10. Gari itatakiwa kuwa na insurance ya hiyo temporary plate ya siku moja au mbili kutegemea utafika lini border
11. Utapatiwa usajili kadi ya gari border ya Tanzania au mkoani na plate number kwa wakala mara nyingi mikoani.
12. Angalizo, fanya utafiti na maafisa wa TRA kuhusu ushuru wa kuingiza hiyo gari kwani system ya TRA haionyeshi kuagiza gari tofauti na nchi gari ilipotengenezwa. Wataingiza kwenye Single Customs Territory system na watakwambia ushuru ni kiasi gani kwani itakuwa chini siyo kama unaagiza kutoka Japan. Ukijua hili ndiyo uanze process nyingine kama inalipa au kuuza huko Burundi na uagize Japan nk au kununua Tanzania gari yenye usajili.