ha haaaa, mngoni mimi natengenezaga mtori......
huo tunakunywa wangoni tu, sithubutu kumkaribisha mchaga, lol!
Ila najua vitu muhimu ni nyama/samaki, ndizi mbichi na viazi kidogo, chumvi.
1. unachemsha nyama/samaki mpaka iive.
2. unaweza hizo ndizi na viazi vinaendelea kuchemka hadi navyo viive. ubakize supu kwa ajili ya kutengenezea mtori
3. huko mijini wengine wanaweka pia caroti, hoho, nyanya........., ila si lazima
4 unatoa zile ndizi na viazi bila supu, unaweka kwenye bakuli unaponda na kijiko. zinapondeka kiurahisi sana kama hazina supu. Ingawa siku hizi watu wanatumia brenda, lol!
5. unaongeza supu kidogo kidogo huku unachanganya upate uji kwa kadiri ya uzito unaotaka. wengine wanarudisha jikoni baada ya kupata huo mtori lakini unaweza kusave baada ya kuchanganya........
huo ndo mtori wa kingoni, lol!