Naomba kujuzwa tofauti kati ya Scania 93m, p94,113 na 124

Naomba kujuzwa tofauti kati ya Scania 93m, p94,113 na 124

d2munisi

Member
Joined
Oct 24, 2011
Posts
7
Reaction score
3
Asalaam aleikum wanafamilia wa Jamii Forums. Leo na mimi nina swali kidogo naomba mwenye uzoefu wa Scania anijuze kidogo. Kuna tofauti gani kati ya hizo Scania hapo juu? Na je kwa kusafirisha mizigo from Mwanza to Dar atleast 3 times a week ipi ambayo itamudu mikiki ya barabara zetu?
 
kwanza sasa hivi hakuna mikiki barabara ni mkeka,pili katika hizo mashine 124 iko sawa na kama una mpunga basi mercedes benz actoss 4853 ndio kiboko yao kwa kuparamia vigongo na kila kitu
 
Kwa sasa barabara sio issue sana , sema hapo issue yako ni reliability ya chombo chenyewe, kutokana na ratiba zako .ie mara 3 kwa wiki fully loaded, hujakuwa specific sana ila nitafanya assuption gari ni kipisi hivyo huvuti trailer.

Ni kwamba 93m na p 94 ni basically kitu kimoja yani zote ni 9000 cc, isipokuwa 94 ni series 4, kwa hiyo kuna mabadiliko kama ,hp katika baadhi ya 94 (210-310 hp), na cabin design .93 ni series 3 . kitaalamu hushauriwi sana kutumia engine ndogo (93 &94 )kwenye mizigo ya kwenda umbali mrefu, unless hiyo gari iwe ilikuwa special kutoka kiwandani. kama ukifuatilia vizuri utaona kuna herufi baada ya hizo namba series 3 walitumia H,-heavy duty , series 4 wametumia L, -long haulage. so kama utafanikiwa kupata 93H au 94L . zinaweza zikafaa kwa kazi zako. 93 m -medium duty ,94d -disribution hazitaadumu kwa safari hiyo unazosema.

113 na 124 ndizo haswa gari unazohitaji kuwa nazo .Tofauti ni kuwa 113 ni 11000cc series 3 ,na 124 ni 12000cc, series 4 .ipo nyingine tena 114 ambayo ni 11000cc series 4 .kimsingi hii ndio ilikuwa update hasa ya 113 .124 ilikuja baadaye sana lengo ni kuongeza ufanisi

113 itakupa maisha marefu ya kazi ngumu , vipuri nafuu na mafundi kila sehemu ,ila ni heavy kwenye matumizi ya mafuta ulilinganisha na 124, inasemekana kwa waliopiga hesabu vizuri waliomiliki gari zote 113 na124 zikifanya kazi ya aina moja kwa pamoja , tofauti ya gharama za mafuta kwa mwaka inaweza kufika lita 3000 mpaka 5000 .124 ikiwa ni economial kuliko 113, penalty inakuja kwenye vipuri ukipata breakdown ya 124 ni ya gharama sana na mafundi wanaozijua ni wachache tena sana , na ni delicate .ila kama utazifuatilia vizuri ni nzuri kuliko 113, na zina lifespan kama 113.

kwa ushauri tu kama unaanza biashara jaribu kutafuta 124L ((360-400 hp) japokuwa ni adimu sana, ila nyingi zilikuwa mechanical injector pump! hapo utapata the best of both world ,economy ya 124 na urahisi wa vipuri wa 113. njia nyingne nikutafuta 113m 320hp nazo pia ni adimu sana ila ni economy ukiliganisha na 113 -360 or 380hp.japo haitafikia 124. ukishindwa hayo ndo utafute hizo 93 na 94 ila unaweza jikuta unatengeneza engine mapema sana , hasa kama mizigoni ni mikubwa ,na schedule ni tight. My favourite lorry of all time ni scania ni 143 na 144L both 14000cc V8 though are heavy on fuel ,but they tend to live forrever if taken care.
 
mdau hapo ameelezea vizuri sana,labda kwa kua ni maelezo marefu unaweza usimpate vizuri, Kwa kifupi ni hivi,
namba ya kwanza ni ujazo wa mafuta kwenye engine, yaani CC, herufi ya pili ni model(wenyewe scania wana ziita series)
92,93,94(9000cc) kwa ajili ya mizigo wastani(na ndizo zitumikazo kwa mabasi).

113,(11,12,13,14,16) ( 11000CC,12000cc...). nguvu ya engine inatofautiana kwa horse power (HP mfano 340,360,380,400,420,470...)

164 500 zinauwezo mkubwa na ndizo hutumika migodini kutoa udongo mawe na vitu vizito chini,

sasa matumiz ya mafuta yanaweza yofautiana kidogo kwa gear 8 na 12,eg kwa km4000 utapata tofauti ya 100lts
 
Mkuu uko loaded vibaya mno..hadi unakera, unajua hadi kupitiliza..mko wawil humu ndani...najipanga nishushe chombo..nikawa tayari tu itabidi niwatafute kwanza mnishauri mawili matatu.
 
Daah watu wanashusha nondo mpaka unawaza mbali na kushangaa haya madude..
 
Kwa sasa barabara sio issue sana , sema hapo issue yako ni reliability ya chombo chenyewe, kutokana na ratiba zako .ie mara 3 kwa wiki fully loaded, hujakuwa specific sana ila nitafanya assuption gari ni kipisi hivyo huvuti trailer.

Ni kwamba 93m na p 94 ni basically kitu kimoja yani zote ni 9000 cc, isipokuwa 94 ni series 4, kwa hiyo kuna mabadiliko kama ,hp katika baadhi ya 94 (210-310 hp), na cabin design .93 ni series 3 . kitaalamu hushauriwi sana kutumia engine ndogo (93 &94 )kwenye mizigo ya kwenda umbali mrefu, unless hiyo gari iwe ilikuwa special kutoka kiwandani. kama ukifuatilia vizuri utaona kuna herufi baada ya hizo namba series 3 walitumia H,-heavy duty , series 4 wametumia L, -long haulage. so kama utafanikiwa kupata 93H au 94L . zinaweza zikafaa kwa kazi zako. 93 m -medium duty ,94d -disribution hazitaadumu kwa safari hiyo unazosema....
hivi kwanini scania kichanja zinapendwa sana?zina nini cha ziada?
 
Back
Top Bottom