Naomba kuuliza kama nitakuwa na hatia

truegooner

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2014
Posts
779
Reaction score
338
Habari zenu. Naombeni kujua kisheria kama nitakuwa na kesi kwenye hili. Mfano, nina ugomvi na mtu, tumepigana kisha akaanza kukimbia nami nikawa namkimbiza. Katika kuvuka barabara yeye haangalii vizuri kama kuna magari, ikatokea akagongwa na kufariki, na watu wameona kabisa kuwa alijiingiza mwenyewe barabarani, je nitakuwa na kesi ya mauaji hapo?
 
Ndyo utakuwa na kosa la kuuwa bila kukusudia ( manslaughter) lakini adhabu hyo inaweza kupunguzwa kutokana na busara ya mahakama kadri itakavyoona inafaa.
 
Ndyo utakuwa na kosa la kuuwa bila kukusudia ( manslaughter) lakini adhabu hyo inaweza kupunguzwa kutokana na busara ya mahakama kadri itakavyoona inafaa.

Asante sana ndugu, je roughly adhabu yenyewe yaweza kuwa miaka mingapi? Yaani miaka miaka mingapi endapo mahakama itakuwa na busara, na endapo haitakuwa na busara ni miaka mingapi roughly? Natanguliza shukrani.
 
Kama nilivyo kwisha sema hutegemea na hekima ya mahakama yenyewe hasa mpaka kufikia kwenye adhabu hyo watakayo itoa. Kuna baadhi ya mashauri yanayofanana na swala lako mahakama zikweza kutoa adhabua ya kifungo cha miaka 30 miaka 5 na wakati mwingine kumwachia kabisa mhusika.. kwa hyo siwezi kutoa adhabu sahihi kuhusu adhabu ila wewe elewa hilo ni kosa kwa mujibu wa sheria .
 

Naomba ushauri Ndugu Yangu alikamatwa na rushwa lakini yeye siye muhusika alikuwa yuko na mwandishi wa habari aliye omba rushwa baadaye mtoa rushwa akampa mtu ambaye akumuomba wakakamatwa wakiwa wote lakini baada ya Ndugu Yangu kuona maafisa wa takukulu wamewavamia akazitupa zile Pesa nje ya ile gorofa waliyokuwepo kupitia dirishani zikadondoka akatumwa afisa wa takukulu kwenda kuzileta alivyo fanikiwa kuzileta wakahakiki zile number kwenye fomu yao waliyokuwa nayo Kisha akaambiwa asaini lakini alikataa na kuwajibu siwezi kusaini kwa sababu amkunikamata na Pesa .
Je hapo anaweza kufungwa?
 
Kwanini alizitupa alipoona maafisa wa takukuru?
Simple alikua anajua mchezo mzima upoje hivyo ananafasi kubwa ya kuwa hatiani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…