Mchuja Nafaka G
JF-Expert Member
- Oct 1, 2014
- 763
- 253
Swali 1: Hivi Outsourcing Company, hupewa leseni kwa sheria ipi ya nchi?
Swali 2: Kwa nini kampuni hizi mfano ISON BPO hulipa mishahara kinyume na maagizo na maelekezo ya serikali?
Mfano, mwaka 2013, serikali kupitia katibu wa Wizara ya Kazi/Ajira, ilitoa agizo na maelekezo kwa ISON BPO, kuwa wao wapo ktk sekta ya mawasiliano kutokana na kazi ambazo wafanyakazi wake wanazifanya.
Kwa maneno mengine inatakiwa walipe mishahara ya kuanzia laki nne kwa wafanyakazi wake, lakini la ajabu kampuni hiyo imekuwa ikitunishia misuli serikali kwa kusisitiza kuwa wao hawapo ktk sekta ya mawasiliano, na imekuwa ikiwalipa wafanyakazi wake mishahara ya kati ya 150,000/- na 270,000/- kama gross salary kwa mwezi.
Je, hii ina maanisha nini?
Swali 3: Kipindi cha majaribio au probationary period ni miezi sita. Kwa namna ninavyoelewa, na baada ya kipindi hicho cha miezi sita, muajiri anatakiwa afanye tathmini ili kuona iwapo mfanyakazi huyo anafaa au la, kama anafaa, muajiri anatakiwa ampe mfanyakazi huyo mkataba wa kazi, na kama mfanyakazi huyo hafai, muajiri inatakiwa amuachishe kazi mfanyakazi.
Lakini ajabu hawa ISON BPO, wamekuwa wakiwatumikisha wafanyakazi wake kwa miaka miwili hadi mitatu bila mikataba, kwa hili sheria inasemaje?
Kwa wasioijua ISON BPO. Hii ni kampuni kutoka India, iliyoingia mkataba na Airtel Tanzania, ili kusimamia kitengo cha huduma kwa wateja kwa mambo ya data, airtelmoney na voice. Na kwa sasa wameingia kampuni ya mawasiliano ya TIGO na kampuni ya ndege ya fastjet kwa vitengo hivyo vya huduma kwa wateja.
*wafanyakazi wanaozungumziwa hapa ni wale wa huduma kwa wateja wa Airtel ila wapo chini ya ISON BPO*
Majibu kitaalamu tafadhalini.
NIMEONA SEHEMU HII HOJA NIMESHINDWA KUWA NA MAJIBU, NAOMBA MSAADA WENU WANAJAMII
Swali 2: Kwa nini kampuni hizi mfano ISON BPO hulipa mishahara kinyume na maagizo na maelekezo ya serikali?
Mfano, mwaka 2013, serikali kupitia katibu wa Wizara ya Kazi/Ajira, ilitoa agizo na maelekezo kwa ISON BPO, kuwa wao wapo ktk sekta ya mawasiliano kutokana na kazi ambazo wafanyakazi wake wanazifanya.
Kwa maneno mengine inatakiwa walipe mishahara ya kuanzia laki nne kwa wafanyakazi wake, lakini la ajabu kampuni hiyo imekuwa ikitunishia misuli serikali kwa kusisitiza kuwa wao hawapo ktk sekta ya mawasiliano, na imekuwa ikiwalipa wafanyakazi wake mishahara ya kati ya 150,000/- na 270,000/- kama gross salary kwa mwezi.
Je, hii ina maanisha nini?
Swali 3: Kipindi cha majaribio au probationary period ni miezi sita. Kwa namna ninavyoelewa, na baada ya kipindi hicho cha miezi sita, muajiri anatakiwa afanye tathmini ili kuona iwapo mfanyakazi huyo anafaa au la, kama anafaa, muajiri anatakiwa ampe mfanyakazi huyo mkataba wa kazi, na kama mfanyakazi huyo hafai, muajiri inatakiwa amuachishe kazi mfanyakazi.
Lakini ajabu hawa ISON BPO, wamekuwa wakiwatumikisha wafanyakazi wake kwa miaka miwili hadi mitatu bila mikataba, kwa hili sheria inasemaje?
Kwa wasioijua ISON BPO. Hii ni kampuni kutoka India, iliyoingia mkataba na Airtel Tanzania, ili kusimamia kitengo cha huduma kwa wateja kwa mambo ya data, airtelmoney na voice. Na kwa sasa wameingia kampuni ya mawasiliano ya TIGO na kampuni ya ndege ya fastjet kwa vitengo hivyo vya huduma kwa wateja.
*wafanyakazi wanaozungumziwa hapa ni wale wa huduma kwa wateja wa Airtel ila wapo chini ya ISON BPO*
Majibu kitaalamu tafadhalini.
NIMEONA SEHEMU HII HOJA NIMESHINDWA KUWA NA MAJIBU, NAOMBA MSAADA WENU WANAJAMII