Wana Jf mimi nina mdogo wangu wa kike ambaye anatatizo la kuota vinyama kama vipele kwenye ngozi then vinakua vikubwa.
Mfano aliota vinyama sehemu aliyotoboa masikio sasa vinazidi kurefuka tu miaka inavyokwenda, pia nyuma ya shingo kimejitokeza kingine bila ya chanzo wala mkwaruzo wowote, hofu yake ni kwamba visije vikazidi au kukua zaidi hapo siku za usoni.
Naomba kujuzwa kwa anayefamu..nini chanzo? Nini tiba au kinga? Wapi anaweza pata msaada wa kitaalamu au kitiba zaidi??
Asanteni.