Naomba majibu juu matumizi ya condom na mwathirika wa UKIMWI

Naomba majibu juu matumizi ya condom na mwathirika wa UKIMWI

Mwashelii

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2013
Posts
477
Reaction score
90
kuingia kwenye mahusiano na mtu aliyeathirika na virusi vya ukimwi pale anapohitaji kujamiiana na asiyeathirika na ugonjwa huo. JE, Condom inaweza kuaminika asilimia mia moja kuwa itazuia maambukizi? Please naomba mnisaidie majibu sahihi.
 
Wakuu mwenzenu ameomba msaada, hivi tunapoambiwa tutumie condom kujikinga na maambukizi si wanamaanisha kuwa kama mtu ana maambukizi na ukajikinga na condom na kuhakikisha kuwa hakuna mkutano wa majimaji ya mwili kati yenu basi mnajikinga na virusi. Hivi mnafikiri mnaweza kuhesabu wanawake/wanaume wote mliolala lao huku wana virusi sema tu mlibahatika kutopata virusi kwa kuwa mlitumia ngono salama?? Mwenzenu hapa anataka apate majibu!!! Hata wenye virusi nao wanahitaji kupata starehe ya tendo la ndoa!!! Aise tumetembea na wenye virusi wengi sema kondomu zilitusaidia sana. Tena bora ufahamu ana virusi ili ujilinde haswa inavyostahili. Kuna wapenzi ninawafahamu, mmoja ana VVU na mwingine hana na wanapendana sana na mapenzi wanafanya kwa tahadhari tena kwa furaha kabisa. Acha kuwanyanyapaaa wenye VVU maana wewe, au wazazi hata watoto wako na ndugu za karibu mnaweza kuupata pia!!! Cha msingi ni vizuri kupimana na mkishafahamu status yenu kama mmoja wenu ni VVU basi mnawaona wataalam wa ushauri nasaha wa VVU katika centres mbalimbali wapo na watawashauri ipasavyo!!! Hapa jamvini watu wanajibu sana kwa kushambulia wakati mmeombwa mtoe ushauri!!! God bless Tanzanians!!! Baki njia Kuu, Acha michepuko!!!! Tuko wangapi???!!!! Je tunabaki njia kuu?? Je tunajua mitungo ya wapenzi wetu!!!!?? Hujafa hujaumbika!!
 
...hata bila condom hupati maambukizi kama upendo wako ni wa dhati,ukimuacha utamnyanyapaa...
 
ama kweli! naona hapa watafiti hawajasema wazi, hebu tunasubili majibu kwako baada ya miezi sita utuambie hapa kama inasaidia au la!
 
UKIMWI haukingiki hata kwa condom za bati-Joseph Haule
 
ukimwi ni ugonjwa wa ki imani ukiamini utaupata na ukiamini hautoupata teh teh aaaahhh,ingawa umdhaniae ndie sie aliye ndie sie aliye sie ndie aliye................
 
Mkuu Mwashelii, mimi sina uhakika na hizi condom za bongo, labda za wenzetu huko majuu, huenda condom zikawa na uwezo wa kumkinga mtu asiambukize/kuambukiza virusi, ila ieleweke ngono ni tendo kubwa linalohusisha viongo mbalimbali vya mwili, mf. wakati wa kumuandaa mwanamke kuna wengne wanatumia ulimi, kunyonyana denda, nk, sina imani na condom za ya uwezo wake wa kuzuia mimba tu, kama condom inazuia maambukizi ya vvu, basi, ujue sio hizi zinazoonekana mitaani ambapo wengine wanapewa bure kama mseto.
 
Haya mapenzi ni hatari!
Hongera sana mkuu.
Nahisi uvaaji wa condom ni ule ule wa kawaida, ukiitumia kwa usahihi inaweza kuzuia maambukizi kwa asilimia kubwa.
 
asanteni sana kwa ushauri wenu Mungu awabariki
. Mimi naona ni vema zaidi nikaenda kwenye vituo vya ushauri nasaha kwa maelezo zaidi.
 
Back
Top Bottom