Naomba majibu kutoka kwa wanasheria

Wakuu mbalimbali naomba nianze kw kuwek baadhi ya vifungu kama ilivyo kwwnye CPA:

"171.-(1) Pale ambapo chini ya masharti ya Sheria hii
mahakama ya chini inayoongozwa na Hakimu wa Wilaya itamtia
hatiani mtu mzima yeyote kwa kosa iwapo, baada ya kupata taarifa
kuhusiana na tabia yake na mengineyo kuhusu mtu huyo mzima au
kuhusiana na mazingira ya kosa, mahakama ina maoni kuwa adhabu
kubwa inatakiwa kutolewa kwa kosa zaidi ya ile ambayo mahakama
ina mamlaka ya kutoa, mahakama inaweza, badala ya kumshughulikia
kwa namna nyingine yoyote, kumweka mhalifu chini ya ulinzi wa
Mahakama Kuu kwa adhabu
kufuatana na masharti yafuatayo ya
kifungu hiki.
(2) Pale ambapo mhalifu anapelekwa Mahakama Kuu kwa
adhabu chini ya masharti ya kifungu hiki,Mahakama Kuu itachunguza
mazingira ya kesi na itamshughulikia mhalifu kwa namna ambayo
mtuhumiwa huyo angeshughulikiwa na Mahakama Kuu iwapo
angetiwa hatiani na Mahakama Kuu kwa kosa hilo."
Lakini ikumbukww kwamba kesi itakua inatajwa tu kutakua hakuna usikilizaji wa shauri katika mahakama ya chini.

Vilevile sijaweka bandiko lolote lenye kuhusianisha sheria na pesa, lahasha mkuu. Nimesema wakili mzuri anawwza kukusaidia kwwnye kesi ngumu. Zingatia kina mzee wa vijisenti, zingatia Lulu and the list continues. Sisi maskini muda mwingne kwa maana ya uchumi tukashindwa kuwapata mawakili wa kutunasua (mana wana gharama kubwa pia) ndo mana tunaanguka.
Nikushukuru mkuu
 
Let me declare my interest if at all I may, mimi sio mwanasheria na chuoni sikusoma sheria. Ila tangu awali nimekua mdau mkubwa sana wa sheria baada ya kuwa forced na circumstances. Ndo mana muda wote, iwe nisimu yangu ama kompyuta, huwa sikosi sheria mbalimbali za nchi hii. I stand for any corrections or amendments kutoka kwa wanasheria na mawakili wasomi waliomo humu jukwaani.
thanking you all
 
Asante mkuu nimekuelewa hapa
 
Mkuu,naomba radhi kwa kuchelewa kujibu kwakuwa nimetingwa na majukumu. Nawahakikishia,nitakuja kujibu maswali kadiri ya uelewa wangu.
 
Wakuu Rweye, chinchilla coat na wengineo,naomba nisajili maoni yangu kwa maswali yalioulizwa. Nitayajibu kwa ujumla kwakuwa natumia simu na inakuwa ngumu kwangu kupanda juu kwenye uzi na kurejea kuandika. Pia,ni vigumu kunakili kila swali.

Mosi,kesi ima ya jinai na madai huongozwa na Sheria na taratibu. Kila nchi ina Sheria zake kuhusu Mamlaka za kuhusika na kesi,utaratibu na hata utekelezaji wa hukumu au uamuzi.

Pili,kwakuwa maswali yahusu jinai na ni kuhusu Tanzania,najikita sasa hapa nchini. Kesi zote za jinai hushughulikiwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini maarufu kama DPP aliye ndani ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Ofisi hiyo husaidiwa na polisi na hata TAKUKURU.

Polisi,pamoja na mambo mengine, hupokea tuhuma;humkamata mtuhumiwa;huandika maelezo ya mtuhumu na mtuhumiwa na kuanza upelelezi. Kabrasha la polisi au TAKUKURU hupelekwa kwa DPP kwa ajili ya kupitiwa na kuandaliwa mashtaka. Mashtaka husomwa mahakamani na kesi huanza. Hapo,mtuhumiwa huwa mshtakiwa.

Tatu,yapo makosa yenye dhamana na yasiyo na dhamana. Makosa yasiyo na dhamana hutajwa na sheria. Mfano,kuua kwa kukusudia,uhaini,ugaidi na kadhalika. Tena,yapo makosa ambayo dhamana yake huweza kuombwa na kutolewa Mahakama Kuu tu. Mfano,uhujumu uchumi na utakatishaji fedha.

Nne,dhamana huombwa. Polisi au mahakama yaweza kukubali au kukataa dhamana kutegemeana na kosa husika,usalama wa mshtakiwa,hali ya kiafya ya muathiriwa, mazingira na tabia ya mshtakiwa na uwezekano wa kuathiriwa kwa upelelezi na ukusanyaji ushahidi kwa ujumla.

Tano,upelelezi ni jambo la kisheria na hufanywa na polisi. Upelelezi waweza kufanyika kabla au wakati wa kesi. Sheria haikuuacha upelelezi uwe wa milele. Imeweka ukomo wa siku 60 isipokuwa tu kama kuna kibali cha kuongeza muda toka kwa DPP. Ukomo unapofika na hakuna nyongeza ya muda,kesi huondolewa na mshtakiwa huachiwa huru.

Sita,DPP amepewa mamlaka ya kuanzisha,kuendeleza,kuondoa,kurudisha,kuunganisha,kusimamisha na kuhamisha kesi yoyote ya jinai. Ndiyo kusema,ana uamuzi wenye baraka za katiba na sheria kushtaki kwa muda atakao na nafasi aipendayo.

Saba,ICC ina utaratibu tofauti na mahakama zetu za ndani. Kwahiyo,leo sitaizungumzia. Lakini,hatukatazwi kuiga mazuri yao.

Nane,kwa kawaida kwenye jinai ni nadra mshtakiwa kupewa tuzo ya kifedha kwa usumbufu na madhila aliyopata wakati kesi inapoisha. Lakini,kama kesi imesikilizwa kikamilifu na kuamuliwa na mahakama yenye uwezo wa kusikiliza na kuamua,aliyekuwa mshtakiwa aweza kufungua shauri la madai kwa msingi wa kushtakiwa kwa hila.

Tisa, kama mshtakiwa ameachiwa kabla ya kusikilizwa kikamilifu kwa kesi yake,aweza kufungua shauri la madai la kushikiliwa isivyo halali kwa usumbufu na madhila yake.

Kumi,nawashukuru na nawatakia siku njema.
 
Asante sana mkuu kwa maelezo mujarabu na hakika umetusaidia wengi. Nilitaka nikusumbue kwenye lile la mwisho la kwanini kesi isianzishwe moja kwa moja kwenye mahakama yenye uwezo wa kusikiliza na kutoa hukumu badala ya kuanzia za chini zisizo na uwezo katika kutoa hukumu ya mwisho? (Mfano za uhujumu na za mauaji)
 
Jambo hilo lipo kisheria. Hupelekwa pale kwa matayarisho yote ya kikesi kama kukusanya ushahidi na kutambua mashahidi. Inapopelekwa Mahakama Kuu,husikilizwa na kutolewa hukumu tu.
 
Umesahau kitu kimoja. Ukipewa dhamana halafu ukarudia kosa hilo hilo uliloshitakiwa ukapata dhamana utaitwa repeat offender dhamana hufutwa iwapo akiomba ifutwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu PETRO E.Mselewa je ukiwekwa mahabusu kisha ukaja kuachiwa bila kupelekwa mahakamani na wewe ukaona umeonewa,je unaweza kufungua kesi ya kudai fidia kwa muda waliokupotezea?
Je hii kesi itakuwa dhidi ya polisi au dhidi ya huyo aliyesababisha ukamatwe au wote kwa pamoja?

“Start where you are. Use what you have. Do what you can.”

 
Mkuu,nimeeleza aya ya pili toka mwisho katika mchango wangu #29. Unawashtaki wote. Yaani aliyesababisha ukamatwe na aliyekukamata na kukushikilia.
 
Mkuu,nimeeleza aya ya pili toka mwisho katika mchango wangu #29. Unawashtaki wote. Yaani aliyesababisha ukamatwe na aliyekukamata na kukushikilia.
Shukrani mkuu na je kuna taratibu gani kwenda kufungua kesi mahakamani bila kupitia polisi?

“Start where you are. Use what you have. Do what you can.”

 
Kuna makosa yameorodheshwa kwenye kifungu 148 cha sheria ya mwenendo wa kesi za jinai kwamba hazina dhamana hivyo mtuhumiwa lazima akae ndani wakati wa kesi.Pili Dpp au mwendesha mashtaka amepewa madaraka makubwa na sheria hivyo ana mamlaka ya kuzuia dhamana ya mtuhumiwa kadri anavyoona.Kumshikilia mtu bila kwenda mahakamani kunakatazwa na sheria kwa mujibu wa Harbeas corpus,hivyo kuna ulazima wa kumpeleka mtuhumiwa mahakamani hata kama ushahid haujakamilika.Pia kwa nji zetu hizi ,taasisi haziko huru,uhuru wa mahakama wenyewe umekabwa na roba za mbao za watawala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shukrani mkuu na je kuna taratibu gani kwenda kufungua kesi mahakamani bila kupitia polisi?

“Start where you are. Use what you have. Do what you can.”
Mkuu,unageuza JF kuwa mahakama na kuharibu uzi wa watu kwa maswali na majibu. Kimsingi,kesi za madai hazipitii polisi. Lakini,waweza kuwapa notisi unaotaka kuwashtaki.
 
Na hii inakiuka Ibara ya 13 ibara ndogo ya 6 kifungu b ya katiba ya jamuhuri ya muungano.Mtuhumiwa hana hatia hadi pale atakapotiwa hatiani na mahakama kwanini kumshikilia? Ikithibitika mahakamani kwamba hana hatia nani atafidia kuzuiliwa kwake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…