Naomba Mawaziri Wengine Waige Mfano wa Dkt Mwigulu Nchemba Pamoja na Dkt Dorothy Gwajima wa kuja kutoa ufafanuzi wa Hoja hapa jukwaani

Naomba Mawaziri Wengine Waige Mfano wa Dkt Mwigulu Nchemba Pamoja na Dkt Dorothy Gwajima wa kuja kutoa ufafanuzi wa Hoja hapa jukwaani

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Nimefurahi sana kuona Mheshimiwa Dkt Mwigulu Lameck Nchemba, Waziri wa Fedha akijitokeza hapa jukwaani kuja kutoa ufafanuzi wa hoja ambayo ilikuwa inagusa wizara yake.Nampongeza sana kwa ujasiri na uthubutu wa hatua hiyo. kwa kuwa hatua hiyo inasaidia kuondoa uzushi , Uongo,taharuki na sintofahamu kwa wananchi.

Ikumbukwe ya kuwa uongo ukiachwa uzungumzwe sana pasipo kujibiwa unaweza kuaminiwa na baadhi ya watu hususani wasio jishughulisha kutafuta ukweli na wakaanza kuamini kuwa ndio ukweli wenyewe.

Ningependa Mawaziri wengine pia Waige Mfano huu uliofanywa na Mheshimiwa waziri .lakini pia napenda kumpongeza sana na kumtia moyo Mheshimiwa Dkt Dorothy Gwajima ambaye yeye sote tunafahamu ya kuwa amekuwa akija bila kusita kutoa ufafanuzi humu jukwaani hususani jukwaa la habari na hoja mchanganyiko.

Tena ingependeza Zaidi wizara zikawa na akaunti zao humu rasmi kwa ajili ya kuelezea masuala mbalimbali yanayokuwa yanatokea au kufanywa katika wizara zao.Lakini siyo tu kuwepo bali kuwa hai wakati wote.

Kikubwa na Rai yangu kwenu waheshimiwa Mawaziri ni kuwa tu na ngozi ngumu kwelikweli muwapo humu jukwaani, maana kuna watu wa kila aina humu jukwaani na wenye lugha za kila aina ambazo zingine unaweza kuhisi kukereka. wavumilieni wote na wala msiwajibu kwa namna watakavyo wajibuni au kuwashambulia.

Maana unaweza ukaandika jambo zuri au ufafanuzi wa jambo zuri halafu ukashangaa mtu anakurukia na kukwambia pasipo ushahidi kuwa wewe ni fisadi,jizi ,mla rushwa na huna akili.kwa hiyo usipo kuwa na kifua na ngozi ngumu utajikuta unapandwa na hasira na jazba na kuzira kabisa kuingia humu jukwaani.Maana wengine unakuta amejaa msongo wa mawazo au ana chuki tu binafsi na wewe au anakuchukia tu bila sababu hata ufanye lipi zuri atakuchukia tu.

Mfano mimi unakuta bila kosa mtu ananitukana matusi ya nguoni kabisa.Lakini huwezi kunikuta nikipaniki au kujibu kwa jazba au kuzira au kuchukia au kurudisha matusi au kumshambulia mtu zaidi ya kujibu kwa busara mfano namwambia mtu kwa upole tu kuwa nimekusame,Mungu Akubariki,asante kwa mtizamo wako,Uwe na Maisha marefu,pole kwa nilipokukwaza,tuvumiliane na kukosoana kwa staha na majibu mengine ya aina hiyo.

Kama waziri unajuwa una presha au hasira au jazba au kukosa subira , uvumilivu na kifua .basi nakushauri usiiingie humu jukwaani kwa jina lako maana utajikuta umejibu watu hovyo na kujipalia mkaa au kujishushia heshima yako na kudharaulika sana.kwa hiyo kama wewe huna kifua na Moyo kama wangu basi ni bora usomage kimya kimya tu na kupita kimya kimya.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimefurahi sana kuona Mheshimiwa Dkt Mwigulu Lameck Nchemba, Waziri wa Fedha akijitokeza hapa jukwaani kuja kutoa ufafanuzi wa hoja ambayo ilikuwa inagusa wizara yake.Nampongeza sana kwa ujasiri na uthubutu wa hatua hiyo. kwa kuwa hatua hiyo inasaidia kuondoa uzushi , Uongo,taharuki na sintofahamu kwa wananchi.

Ikumbukwe ya kuwa uongo ukiachwa uzungumzwe sana pasipo kujibiwa unaweza kuaminiwa na baadhi ya watu hususani wasio jishughulisha kutafuta ukweli na wakaanza kuamini kuwa ndio ukweli wenyewe.

Ningependa Mawaziri wengine pia Waige Mfano huu uliofanywa na Mheshimiwa waziri .lakini pia napenda kumpongeza sana na kumtia moyo Mheshimiwa Dkt Dorothy Gwajima ambaye yeye sote tunafahamu ya kuwa amekuwa akija bila kusita kutoa ufafanuzi humu jukwaani hususani jukwaa la habari na hoja mchanganyiko.

Tena ingependeza Zaidi wizara zikawa na akaunti zao humu rasmi kwa ajili ya kuelezea masuala mbalimbali yanayokuwa yanatokea au kufanywa katika wizara zao.Lakini siyo tu kuwepo bali kuwa hai wakati wote.

Kikubwa na Rai yangu kwenu waheshimiwa Mawaziri ni kuwa tu na ngozi ngumu kwelikweli muwapo humu jukwaani, maana kuna watu wa kila aina humu jukwaani na wenye lugha za kila aina ambazo zingine unaweza kuhisi kukereka. wavumilieni wote na wala msiwajibu kwa namna watakavyo wajibuni au kuwashambulia.

Maana unaweza ukaandika jambo zuri au ufafanuzi wa jambo zuri halafu ukashangaa mtu anakurukia na kukwambia pasipo ushahidi kuwa wewe ni fisadi,jizi ,mla rushwa na huna akili.kwa hiyo usipo kuwa na kifua na ngozi ngumu utajikuta unapandwa na hasira na jazba na kuzira kabisa kuingia humu jukwaani.Maana wengine unakuta amejaa msongo wa mawazo au ana chuki tu binafsi na wewe au anakuchukia tu bila sababu hata ufanye lipi zuri atakuchukia tu.

Mfano mimi unakuta bila kosa mtu ananitukana matusi ya nguoni kabisa.Lakini huwezi kunikuta nikipaniki au kujibu kwa jazba au kuzira au kuchukia au kurudisha matusi au kumshambulia mtu zaidi ya kujibu kwa busara mfano namwambia mtu kwa upole tu kuwa nimekusame,Mungu Akubariki,asante kwa mtizamo wako,Uwe na Maisha marefu,pole kwa nilipokukwaza,tuvumiliane na kukosoana kwa staha na majibu mengine ya aina hiyo.

Kama waziri unajuwa una presha au hasira au jazba au kukosa subira , uvumilivu na kifua .basi nakushauri usiiingie humu jukwaani kwa jina lako maana utajikuta umejibu watu hovyo na kujipalia mkaa au kujishushia heshima yako na kudharaulika sana.kwa hiyo kama wewe huna kifua na Moyo kama wangu basi ni bora usomage kimya kimya tu na kupita kimya kimya.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
hakika umejua kutoa andiko lenye mashiko
 
Sasa matusi ya nini ndugu yangu mtanzania uliyejaa msongo wa mawazo au umetoka bar ukiwa upo na kilevi kichwani😀😀😀 .Daa kweli Jamii forum inahitaji mtu kuwa na ngozi ngumu na uvumilivu na moyo wa kusamehe.sasa hapa nimefanya kosa gani hadi unitukane?😀😀 Ok nimekusamehe bure kabisa
Wewe ni mnafiki mkubwa ktk nchi hii.. na nakwambia hutafika mbali.
 
Huyo mzee wa fedha ametoa ufafanuzi upi??
 
Mbali wapi huko unako kuzungumzia? Kwanini wewe ndiye unasafirisha watu?
Wewee..
We kula tu saivi.. ila walikuwepo wenzako humu. Saivi wako kimya na wamewageuka.

So when its your time to eat..eat. Ila usitusumbue.
 
Wewee..
We kula tu saivi.. ila walikuwepo wenzako humu. Saivi wako kimya na wamewageuka.

So when its your time to eat..eat. Ila usitusumbue.
Nani amekuweka humu jukwaani na kukulipa kutukana matusi watu kama vile kichaa au mwendawazimu?
 
We Lucka tutakusomea kurjuaaaani haiwezani shida zote hizi we ni kusifia tuuu haya juzi Nape kahara hujayaona hayo? Ufisadi uliokithiri pamoja na ukosefu wa huduma muhimu za kijamii huoni hayo? Hata vitoto vyetu masikini bima vimetolewa sijui wameviona ni viroboti haviumwi wewe kila siku ni kusifiaaaa tuuu
 
We Lucka tutakusomea kurjuaaaani haiwezani shida zote hizi we ni kusifia tuuu haya juzi Nape kahara hujayaona hayo? Ufisadi uliokithiri pamoja na ukosefu wa huduma muhimu za kijamii huoni hayo? Hata vitoto vyetu masikini bima vimetolewa sijui wameviona ni viroboti haviumwi wewe kila siku ni kusifiaaaa tuuu
Ufisadi upi unaouzungumzia ndugu yangu mtanzania? Huduma kwa sasa zimesogezwa karibu kabisa ya mwananchi.ndio maana hakuna wanaotembea umbali mrefu kufuata na kutafuta huduma kama vile maji au zahanati au kituo cha afya.hata wanafunzi hawatembei umbali mrefu kwenda shule maana shule zipo mirangoni mwao
 
Labda Gwajima, lakini Mwigulu ametoa ufafanuzi gani wa maana? Posts zake zote alizotoa hivi karibuni zinaingia akili kwa wasio na uelewa tu
 
Back
Top Bottom