Naomba msaa jamani maana mama yangu kadhalilishwa.

Sezariziki

Member
Joined
Jul 10, 2013
Posts
35
Reaction score
2
Kuna mama jirani yetu kamuibulia mama yetu madai anamuibia mumewe bila ya kuwa na ushahidi wowote. Na kutokana na hilo amewapigia simu watoto wake na kuwapa uongo huo,hatimaye watoto wa yule mama wameishia kutuma maneno machafu na matusi,kwa kweli kimeniuma maana wamemdhalilisha mama yangu bila hatia. Wadau hapa sheria inasemaje juu ya kumtusi mtu,nashindwa nianzie wapi.
 
Kama mna ushahidi wa hayo matusi, ni vema kuripoti polisi.
 
Kama mama yako hajatembea na huyo baba yao bora muachane nao tu, wachukulieni kama watoto wasio na adabu. Matusi hayajeruhi
.
 

Je mama yako alishawahi kulaumiwa kuhusiana na hii hali ya uzinzi au ndio mara ya kwanza? kama ndo mwanzo wapotezeeni ila kama ilishawahi tokea muonye mamayo..
 
Kwa sheria za nje ni kosa kumtusi mtu hata kama ana makosa na huyo mama kama ana ushaid anatakiwa kwenda mahakamani na ushaid wake pili nawe mchunguze mama yako kama kweli hajatembea na jirani yake maana ukweli wanaujua wao wawili na mungu wao.
 
Je mama ako anaishi chini ya paa moja la nyumba ya kupanga na huyo jirani?
Je anafanya biashara ya aina moja na jirani?
Je kuna shughuli zozote za kutafuta kipato walizokuwa wakishirikiana kabla ya maneno kuzuka?

Endapo ndio huenda ni njia mojawapo ya kutafuta utengano?

Endapo hapana basi anayejua ukweli ni mama ako na hawezi kukwambia
 
kwenye sheria kuna kitu inaitwa defarmation,sasa inategemea kama ushahd upo,unaweza kwenda kushitaki mahakamani lkn ni jukumu la mama yako kuprove kwamba maneno hayo ni ya uongo na hayana ukweli wowote na pia yamemshushia heshima kiasi gani katika jamii inayomzunguka
 

Hao watoto wa huyo mama wapo mkoani na walitukana na kutoa maneno yao kutoka huko cha ajabu mimi nimefunga safari nimekuja huku WAO wamegoma kuja kusuluhisha kindugu na mama yao kagoma kusema anaushaidi gani sasa me naona dawa yao ni sheria kufuata mkono tu.
 
Je mama yako alishawahi kulaumiwa kuhusiana na hii hali ya uzinzi au ndio mara ya kwanza? kama ndo mwanzo wapotezeeni ila kama ilishawahi tokea muonye mamayo..

Mama yangu hana hiyo historia na wala sijawahi kuhisi hilo jambo kipindi chote yaani limetokea ghafla na chanzo ni wivu wa maendeleo...kuna watu wanatamani wakuone ukiwa na hali hiyo hiyo miaka yote.
 
ni vigumu kutoa ushauri hapa, kwasababu anayeongea siye aliyedhalilishwa, bali mtoto wa aliyedhalilishwa. angeliongea mama yako hapa, tungesema vingine, lakini unaongea wewe tena kuhusu mama yako. kwani kama ni kweli mama yako aliteleza kwa kosa hilo, unafikiri angekuja kukuaga wewe kama anaenda, au angekueleza wewe mtoto wake kwamba anafanya jambo kama hilo, jambo hilo huwa linafanyika kwa siri na si hadharani ikizingatia tena mme wa mtu...nashauri usilipuke sana kumtetea mama yako, wakati mwingine huwa inawezekana hao watu wakawa na ushahidi mzuri tu, either wa meseji walizoandikiana, au wa picha kukutwa laivu, na mambo mengine mengi tu ambayo wanaweza wakawa hawajayatoa hadharani. wanapata wapi ujasiri wa kusambaza habari hizo hadi kuwaambia watoto wake? tuseme kweli hawana akili timamu hata wakachukua uamzi mzito kama huo? lazima kuna sababu tu, kaeni chini mjichunguze kabla ya kuchukua hatua. what if ninyi mkienda kufungua kesi ya defamation ili mama yako alipwe kwa kudhalilishwa na kuchafuliwa reputation? halafu wao wakaja na ushahidi mzurii ulionyooka kuonyesha kuwa kitu hicho kilikuwa cha kweli? si itakuwa aibu mara mbili? nashauri mama yako ajichunguze, akae chini ajichunguze kabisaaa, ajiulize kwanini asingiziwe yeye tu tena na mume wa mtu jambo ambalo si la kawaida, baada ya hapo, kama kweli, mbele za Mungu atakuwa na uhakika kuwa kadhalilishwa bila sababu yeyote, afanye haya hapa chini.

kudhalilishwa kwa kuchafuliwa jina mbele za watu ni tort ya defamation, anaweza kufungua kesi ya madai mahakamani. lakini ajabu yake, dafamation ina defence mojawapo kuwa, kama kitu kilichosemwa ni cha ukweli, basi hawezi kuja kushinda hiyo kesi, ndio maan anasema isije kuwa wanao ushahidi wameuhifadhi, wameanza tu kubip ili mtu akipiga wao wamwage kabisa ugali na mboga, kama ni kitu cha kweli mtaumbuka. kama mama yako anahisi ni kweli kuna jambo hilo, potezeeni, endeleeni na maisha wala msipoteze muda nao.

vilevile, kama kuna matusi yameandikwa either kwenye msg za simu, au kuna ushahidi wa kutosha wa kuvurumishiwa matusi na mnao mashahidi, mnaweza kwenda kurepoti polisi ili afunguliwe kesi ya jinai. lakini mkishaanza hayo yote, jueni kuwa mpo vitani, mnapambana na watu, ama zao ama zenu. mnaweza kushangaa mnavyozidi kupambana nao ndivyo mnavyozidi kumtangaza mama yenu na kusambaza uzushi huo zaidi, kukawa hasara zaidi kuliko faida...na mama yetu hadi aje asafishe jina miaka kibao itapita.

kuna jamaa yangu mmoja alishawahi kuzushiwa jambo kama hilo, alivyozidi kupambana na wale watu, ndivo habari zilivyozidi kusambaa zaidi, kama angelinyamaza zisingesambaa. au, aende kwa wazee aombe msamaha kama alifanya. kama hakufanya, pia aende kwa wazee wawakalishe ili wamwambia huyo mama asiendelee kusambaza uzushi. poleni sana, ila nakushauri usimtetee sana mama yako, kwasababu yeye ni mtu mzima, na asingeaga anapoenda kufanya jambo zuru au baya....samahani kama nitakuwa nimekukwaza.

View attachment 102822

View attachment 102822View attachment 102822
View attachment 102821View attachment 102821View attachment 102821
 
This is pure defamation (in the presence of evidences).So sorry
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…