Naomba msaada kuku kuvimba macho na kutoa uchafu wa majimaji kama ya sabuni

Naomba msaada kuku kuvimba macho na kutoa uchafu wa majimaji kama ya sabuni

vakolavene

Member
Joined
Jan 20, 2017
Posts
39
Reaction score
26
Habari za muda huu naomba msaada ni tiba gani inafaa kwa kuku wanaofunga macho na kutoa uchafu km maji ya sabuni ya kipande ilio lowekwa. (Ulenda ulenda).

Na huu ugonjwa unatokana na nini pia unasababishwa na nn? maana kuna baadhi ya kuku wangu wameanza kua na ugonjwa huu inanikosesha raha kabisa mana hawana raha na wanajitenga peke yao macho hufanana na hivi
images-3.jpeg
 
Homa ya mafua! Wape dawa inaitwa trimazin itawasaidia! Hakikisha kuna udafi bandani pia waliona na ugonjwa hyo watenge peke yao na uwatibie
Mdau Samahani bumblefoot na fungus ni sawa dawa yake nini
 
Kaka Pole Yaani Hilo Tatizo nilikuwa nalo pia katika enzi za ufugaji
Ila Nikupe siri moja tu madawa ya kisasa mara nyingi hayana nguvu sana ya kutibu kuku akiwa katika hali ya kuumwa
bali chanjo ndio inakuwa na nguvu kuliko tiba.
Mimi NIlitumia njia hizi za Asili Nilizofundishwa na Mfugaji Mmoja Ni nzuri na Zinasaidia Sana

1.Hakikisha kwanza Unawatenga hao kuku katika sehemu yao maana huo ugonjwa huwa unaambukiza japo hauna nguvu sana ya kusambaa ila ukikolea ni hatari kwa mifugo.

2.Chukua pamba stiki (zamasikioni zile ambazo ni ngumu sio zile laini za watoto) Unachukua na maji ya uvuguvugu unatumia hiyo pamba stik kwa kuilowesha katika maji mara kwa mara kisha unawasaidia kuwasafisha macho kwa kuwafuta kwa kutumia hiyo(Kwa utaratibu sana bila kuwaumiza)
hakikisha unakuwa umekaa kwenye kigoda au stull kisha kuku unamshika vizuri kabisa ali usimuumize
Unaweza ona papo hapo mabadiriko hayo ya kuku kupata nafuu

3.Chukua vitunguuu Swaumu Kadhaa vimenye kisha Changanya Katika maji Kisha Mnyweshe Kijiko Kimoja Cha Chakula hata viwili(Haia Madhara Hata akinywa vinne Ila NI vizuri kumpa tu Viwili Au Kimoja Kulingana na Ukubwa wa Kuku Zaidi ya Umri wa Miezi 3 Mpe Viwili)

4.Utafanya hivyo Kila Asubuhi Na huku Kila Baada ya masaa kama matatu unakuwa unawaangalia kuku mara kwa mara ili ujue nini maendeleo yao(Mimi Nilikuwa natumia hata zaidi ya lisaa limoja kusoma tabia za kuku na kujua yupi mkorofi yupi dhaifu maana wakati mwingine kuku anakuwa anatembea lakini ni mgonjwa mpaka uwe umekaa naye kwa mad ndio utajua mapungufu yake)

Ukifuata vizuri hivyo ni ndani ya siku 1-3 Kuku wanakuwa level nyingine kabisa
napia hata Kwa Kuku ambao ni wazimaUnawafanyia Kitunguu swaumu unawanywesha kila Asubuhi kwa Siku tau mfululizo na siku zinazofuati aunawachanganyihia katika majiyao ya kunywa.
hope umepata Kitu
 
Kaka Pole Yaani Hilo Tatizo nilikuwa nalo pia katika enzi za ufugaji
Ila Nikupe siri moja tu madawa ya kisasa mara nyingi hayana nguvu sana ya kutibu kuku akiwa katika hali ya kuumwa
bali chanjo ndio inakuwa na nguvu kuliko tiba.
Mimi NIlitumia njia hizi za Asili Nilizofundishwa na Mfugaji Mmoja Ni nzuri na Zinasaidia Sana

1.Hakikisha kwanza Unawatenga hao kuku katika sehemu yao maana huo ugonjwa huwa unaambukiza japo hauna nguvu sana ya kusambaa ila ukikolea ni hatari kwa mifugo.

2.Chukua pamba stiki (zamasikioni zile ambazo ni ngumu sio zile laini za watoto) Unachukua na maji ya uvuguvugu unatumia hiyo pamba stik kwa kuilowesha katika maji mara kwa mara kisha unawasaidia kuwasafisha macho kwa kuwafuta kwa kutumia hiyo(Kwa utaratibu sana bila kuwaumiza)
hakikisha unakuwa umekaa kwenye kigoda au stull kisha kuku unamshika vizuri kabisa ali usimuumize
Unaweza ona papo hapo mabadiriko hayo ya kuku kupata nafuu

3.Chukua vitunguuu Swaumu Kadhaa vimenye kisha Changanya Katika maji Kisha Mnyweshe Kijiko Kimoja Cha Chakula hata viwili(Haia Madhara Hata akinywa vinne Ila NI vizuri kumpa tu Viwili Au Kimoja Kulingana na Ukubwa wa Kuku Zaidi ya Umri wa Miezi 3 Mpe Viwili)

4.Utafanya hivyo Kila Asubuhi Na huku Kila Baada ya masaa kama matatu unakuwa unawaangalia kuku mara kwa mara ili ujue nini maendeleo yao(Mimi Nilikuwa natumia hata zaidi ya lisaa limoja kusoma tabia za kuku na kujua yupi mkorofi yupi dhaifu maana wakati mwingine kuku anakuwa anatembea lakini ni mgonjwa mpaka uwe umekaa naye kwa mad ndio utajua mapungufu yake)

Ukifuata vizuri hivyo ni ndani ya siku 1-3 Kuku wanakuwa level nyingine kabisa
napia hata Kwa Kuku ambao ni wazimaUnawafanyia Kitunguu swaumu unawanywesha kila Asubuhi kwa Siku tau mfululizo na siku zinazofuati aunawachanganyihia katika majiyao ya kunywa.
hope umepata Kitu
Asante
 
Napia Kuku Wakiwa na Mafua Kitunguu Swaumu Unatumia kama Nilivyokuelekeza Hapo juu
Kitunguu Swaumu hutibu Zaidi ya Magonjwa 18+ Ya Kuku na Pia huwa Ni Kinga nzuri sana kwa kuku kwa wakati wote.

kumsaidia kuku anayeumwa mafua

Kuku akiumwa mafua yaani hapa anakuwa kama mzungu huu ni ugonjwa mbaya sana kwakuku hata ukimuona unamuonea huruma kabisa na hu ni ugonjwa unaoua kimya kimya kuku mara nyingi unaamka asubuhi unakuta kuku kakauka tayari na Mara nyingi huwa unaambukiza kwa kasi kidogo usipowawahishia tiba.
na Ukiwa umemwanzishia dozi ya kitunguu swaumu basi kuku hawezi kueneza hayo mafua kwa wengine(Na Hao Wengine Ukiwa umewawekea utaratibu wa kunywa kitunguu swaumu katika maji yao)

1.Chukua stiki ile ya kujichokonolea kwenye meno ukila nyama ikanasia ama kitu chochote japo wengine huweka kama pambo tu Unamshika kuku unamwangaliza kwa mbele ukiwa umekaa katika kigoda au stull(kimo hicho ndio utamsaidia kuku vizuri) Mkia wake unakuwa tumboni kwako na kichwa mbele basi unamshika kichwa unakuwa unamsaidia kuzibua pua maana mara nyingi huwa zinaziba.
Unazibua kwa kubonyeza juu ya pua ya kuku kama unapangusa hivi ukitumia pembeni sio kwenye ncha(Mfano kama mama anavyosukuma chapati vile ndio unatumia pembeni humo mwa stiki kubonyeza pua a kuku na utaona mafua uchaufu ukitoka ambao ulikuwa umeziba) Huku akimnywesha kitunguu swaumu

2.mara zote kuku pua zikiziba utamtambua atakuwa ni mpole sana na anakuwa anatabia kama ya kupiga chafya mara kwa mara huku akizungusha kichwa chake, Mda mwingine huchokonoa kwa kutumia makucha yake japo huwa hafanikiwi mara zote, huwa hali sababu anakosa uwezo wa kupumua vizuri ukimshitua mara moja unamuona anachanamka kidogo lakini ndani ya dakika hiyo hiyo anaduwaa tena haendelei kula.
basi Utajua tuu huyu shida ni hiyo na utamsaidia kama hapo mwanzo.

Kuku kufuga ni raha sana yaani asikuambie mtu ila wakiwa na usimamizi mzuri
Nimefuga sana kuku ila madawa ya kisasa mengi huwa yanguvu katika kinga kuliko tiba
na tiba nzuri ipo kienyeji kuliko kisasa

Namimi NIlifuga sana Kuku wa Kienyeji Kuliko Wa Kisasa Maana Wakienyeji Walikuwa na Faida Kubwa Kwangu

napia Kuku wa Kienyeji Sio Ndio Anastahimili Sana magonjwa bali Ukipata Kuku Chotara Jogoo wakisasa+Teta Wakienyeji=Product yake Ndio Hustahimili Zaidi magonjwa
 
Napia Kuku Wakiwa na Mafua Kitunguu Swaumu Unatumia kama Nilivyokuelekeza Hapo juu
Kitunguu Swaumu hutibu Zaidi ya Magonjwa 18+ Ya Kuku na Pia huwa Ni Kinga nzuri sana kwa kuku kwa wakati wote.

kumsaidia kuku anayeumwa mafua

Kuku akiumwa mafua yaani hapa anakuwa kama mzungu huu ni ugonjwa mbaya sana kwakuku hata ukimuona unamuonea huruma kabisa na hu ni ugonjwa unaoua kimya kimya kuku mara nyingi unaamka asubuhi unakuta kuku kakauka tayari na Mara nyingi huwa unaambukiza kwa kasi kidogo usipowawahishia tiba.
na Ukiwa umemwanzishia dozi ya kitunguu swaumu basi kuku hawezi kueneza hayo mafua kwa wengine(Na Hao Wengine Ukiwa umewawekea utaratibu wa kunywa kitunguu swaumu katika maji yao)

1.Chukua stiki ile ya kujichokonolea kwenye meno ukila nyama ikanasia ama kitu chochote japo wengine huweka kama pambo tu Unamshika kuku unamwangaliza kwa mbele ukiwa umekaa katika kigoda au stull(kimo hicho ndio utamsaidia kuku vizuri) Mkia wake unakuwa tumboni kwako na kichwa mbele basi unamshika kichwa unakuwa unamsaidia kuzibua pua maana mara nyingi huwa zinaziba.
Unazibua kwa kubonyeza juu ya pua ya kuku kama unapangusa hivi ukitumia pembeni sio kwenye ncha(Mfano kama mama anavyosukuma chapati vile ndio unatumia pembeni humo mwa stiki kubonyeza pua a kuku na utaona mafua uchaufu ukitoka ambao ulikuwa umeziba) Huku akimnywesha kitunguu swaumu

2.mara zote kuku pua zikiziba utamtambua atakuwa ni mpole sana na anakuwa anatabia kama ya kupiga chafya mara kwa mara huku akizungusha kichwa chake, Mda mwingine huchokonoa kwa kutumia makucha yake japo huwa hafanikiwi mara zote, huwa hali sababu anakosa uwezo wa kupumua vizuri ukimshitua mara moja unamuona anachanamka kidogo lakini ndani ya dakika hiyo hiyo anaduwaa tena haendelei kula.
basi Utajua tuu huyu shida ni hiyo na utamsaidia kama hapo mwanzo.

Kuku kufuga ni raha sana yaani asikuambie mtu ila wakiwa na usimamizi mzuri
Nimefuga sana kuku ila madawa ya kisasa mengi huwa yanguvu katika kinga kuliko tiba
na tiba nzuri ipo kienyeji kuliko kisasa

Namimi NIlifuga sana Kuku wa Kienyeji Kuliko Wa Kisasa Maana Wakienyeji Walikuwa na Faida Kubwa Kwangu

napia Kuku wa Kienyeji Sio Ndio Anastahimili Sana magonjwa bali Ukipata Kuku Chotara Jogoo wakisasa+Teta Wakienyeji=Product yake Ndio Hustahimili Zaidi magonjwa
Mkuu kuku wangu anakohoa kinoma yaani, nitumie njia gani kumsaidia

Slippy Gerald, you served football.
 
Napia Kuku Wakiwa na Mafua Kitunguu Swaumu Unatumia kama Nilivyokuelekeza Hapo juu
Kitunguu Swaumu hutibu Zaidi ya Magonjwa 18+ Ya Kuku na Pia huwa Ni Kinga nzuri sana kwa kuku kwa wakati wote.

kumsaidia kuku anayeumwa mafua

Kuku akiumwa mafua yaani hapa anakuwa kama mzungu huu ni ugonjwa mbaya sana kwakuku hata ukimuona unamuonea huruma kabisa na hu ni ugonjwa unaoua kimya kimya kuku mara nyingi unaamka asubuhi unakuta kuku kakauka tayari na Mara nyingi huwa unaambukiza kwa kasi kidogo usipowawahishia tiba.
na Ukiwa umemwanzishia dozi ya kitunguu swaumu basi kuku hawezi kueneza hayo mafua kwa wengine(Na Hao Wengine Ukiwa umewawekea utaratibu wa kunywa kitunguu swaumu katika maji yao)

1.Chukua stiki ile ya kujichokonolea kwenye meno ukila nyama ikanasia ama kitu chochote japo wengine huweka kama pambo tu Unamshika kuku unamwangaliza kwa mbele ukiwa umekaa katika kigoda au stull(kimo hicho ndio utamsaidia kuku vizuri) Mkia wake unakuwa tumboni kwako na kichwa mbele basi unamshika kichwa unakuwa unamsaidia kuzibua pua maana mara nyingi huwa zinaziba.
Unazibua kwa kubonyeza juu ya pua ya kuku kama unapangusa hivi ukitumia pembeni sio kwenye ncha(Mfano kama mama anavyosukuma chapati vile ndio unatumia pembeni humo mwa stiki kubonyeza pua a kuku na utaona mafua uchaufu ukitoka ambao ulikuwa umeziba) Huku akimnywesha kitunguu swaumu

2.mara zote kuku pua zikiziba utamtambua atakuwa ni mpole sana na anakuwa anatabia kama ya kupiga chafya mara kwa mara huku akizungusha kichwa chake, Mda mwingine huchokonoa kwa kutumia makucha yake japo huwa hafanikiwi mara zote, huwa hali sababu anakosa uwezo wa kupumua vizuri ukimshitua mara moja unamuona anachanamka kidogo lakini ndani ya dakika hiyo hiyo anaduwaa tena haendelei kula.
basi Utajua tuu huyu shida ni hiyo na utamsaidia kama hapo mwanzo.

Kuku kufuga ni raha sana yaani asikuambie mtu ila wakiwa na usimamizi mzuri
Nimefuga sana kuku ila madawa ya kisasa mengi huwa yanguvu katika kinga kuliko tiba
na tiba nzuri ipo kienyeji kuliko kisasa

Namimi NIlifuga sana Kuku wa Kienyeji Kuliko Wa Kisasa Maana Wakienyeji Walikuwa na Faida Kubwa Kwangu

napia Kuku wa Kienyeji Sio Ndio Anastahimili Sana magonjwa bali Ukipata Kuku Chotara Jogoo wakisasa+Teta Wakienyeji=Product yake Ndio Hustahimili Zaidi magonjwa
[emoji736] [emoji736] safi mkuu dawa za asili ni nzuri sana zipo nyingi alaf zinapatikana kirais na sio bei na zinamatokea ya fast

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kuku wangu anakohoa kinoma yaani, nitumie njia gani kumsaidia

Slippy Gerald, you served football.


Tumia Maelezo Kama nilivyoonyesha hapo juu Tumia Kitunguu Swaumu Hayo ni Mafua Yanaanza Na Yanaweza Kuenea Kwa Kuku wengine

EPUKA YAFUATAYO
1. Kununua kuku katika minada na kuleta bandani
2. Kuruhusu kila mtu kuingia katika banda la kuku
3. Kuacha mabaki ya kuku walikufa ovyo katika mazingira ya kuku
pia,endapo kuku wengi walikufa katika banda hilo basi ni vyema usilete kuku wengine katika banda hilo angalau kwa ,mwezi au zaid.
4. Tenganisha kuku wenye dalili za ugonjwa na kuku wengine.
5. ZINGATIA USAFI WA BANDA NA VYOMBO VYA KUKU WAKO.


Mambo ya kuzingatia
-safisha banda wanalolala na kisha mwaga majivu ya moto kwa kuzungusha katika kona za chini na kufuata ukuta ulivyo.
-Kule kwetu unyakyusani kuna miti inaitwa Mifungula inamitunda fulani hivi mikubwa sana inakuwa kama mhogo ila inakuwa ninaning'inia cukua hata mitano hiyo itengeneze kama mtumbwi kisha wawekee maji ya kunywa humo walau siku 7-11 mfululizo
 
Mkuu kwa uzoefu wangu hiyo pia inaweza kuwa ni dalili ya kuku kukosa vitamin. Ukienda kwa wataalamu wanaweza kukwambia dawa nzuri ya kutumia. Ila uwe unawalisha na mchicha nao unasaidia sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za muda huu.
Naomba msaada ni tiba gani inafaa kwa kuku wanaofunga macho na kutoa uchafu km maji ya sabuni ya kipande ilio lowekwa. (Ulenda ulenda). Na huu ugonjwa unatokana na nn?
Pia unasababishwa na nn?
Mana kuna baadhi ya kuku wangu wameanza kua na ugonjwa huu. Inanikosesha raha kabisa mana hawana raha na wanajitenga peke yao.
Macho hufanana na hivi
View attachment 536827
Mafua hayo tumia fluban siku tatu kwisha kazi wala usiogope,
 
Habari za muda huu.
Naomba msaada ni tiba gani inafaa kwa kuku wanaofunga macho na kutoa uchafu km maji ya sabuni ya kipande ilio lowekwa. (Ulenda ulenda). Na huu ugonjwa unatokana na nn?
Pia unasababishwa na nn?
Mana kuna baadhi ya kuku wangu wameanza kua na ugonjwa huu. Inanikosesha raha kabisa mana hawana raha na wanajitenga peke yao.
Macho hufanana na hivi
View attachment 536827
Mkuu; Pata ushauri wa kitaalam(Waone mabw. au maBi.mifugo) walio katika eneo lako. Kwa namna ulivyoeleza yawezekana ikawa ni Ndui ya kuku (Chicken pox) na huo ugonjwa husababishwa na virus (it is a Viral disease) - hauna dawa ya tiba ila chanjo ipo. Kuku wanakufa kutokana na macho kufunga na hivyo kuku anashindwa kuona chakula na hapohapo magonjwa nyemelezi hususan Bacterial diseases huibuka na ndiyo yanayosababisha kuku kufa. Cha kufanya: Jitahidi kusafisha macho ya kuku walioathirika kwa maji ya uvuguvugu yaliyochanganywa na chumvi (chumvi ya jikoni) kwa kutumia pamba zile za kusafisha masikio kisha uwapake antibiotic e.g. oxytetracycline eye ointment.
 
Tatizo la kuvimba macho linatokana na upungufu wa protini
 
habari viongozi kuku wangu wana vidonda kwenye mdomo pembeni pia wanatabia ya kula vidole vyao vya miguu je t inaweza kuwa ni tatizo gani
 
Wachinje tembeza nyama bar za Sinza, hutajuta watanunuliwa wote utakuwa ume save gharama za dawa, na muda wa kuwahudumia.
 
Back
Top Bottom