Baada ya kunyonyolewa muweke sehemu yenye nafasi tumia sinia au hata mezani, anza na kutoa kivuko cha chakula (uchafu pale shingoni, kivute vizuri kisitumbuke, akiwa chali toa paja na t.a.k. (yaani hips) mgeuze kifudifudi kama si mtaalam papasa katikati ya bega lake na mgogo kuna kifupa utakishika ingiza kisu sehemu hiyo pandisha juu kwenye maungio ya kipapatio kivunje toa pamoja na kipapatio halafu ingiza vidole gumba sehemu ulipotoa kipapatio (mshike mkono wako mmoja upande wa kifua mwingine upande wa mgongo) tenganisha tumbo na mgongo, vitu vyote vya ndani vitakuwa sehemu ya mgongo vitoe kwa pamoja kata vizuri nnya izidondokee kwenye nyama, tenganisha kiuno na kila wajinga (mbavu) hakikisha huyo kuku katoka vipande 9: paja 2, t.a.k.o (hips) 2, mgongo, mbavu (mgongo na mbavu hazikatwi mara mbili) vipapatio (mbawa)2, Steki ya tumbo 2. shingo peke yake 1. kama mlaji wa filigisi itumbue vizuri usitenganishe na maini hakikisha umetoa kifuko cha nyongo. hapo umemaliza kazi endelea na upishi wako.