Naomba msaada wa kisheria au mawazo dhidi ya mwenye nyumba wangu

Naomba msaada wa kisheria au mawazo dhidi ya mwenye nyumba wangu

Zee la choji

Member
Joined
May 15, 2016
Posts
56
Reaction score
122
Habari za muda huu?

Nilitafutiwa chumba na dalali maeneo ya Magomen Kagera pale maeneo ya Oil com, Hivyo basi nilitoa kodi ya miez 5 na Kodi ya 1 ya dalali jumla nikatoa tsh 360,000 kwasababu kodi ya chumba ilikuwa tsh 60,000.

Sasa baada ya wiki moja alikuja mtu wa makamo na kujitambulisha kuwa yeye ni mwenye nyumba, na hiyo nyumba ni ya kwake alinunua na ipo kwenye mgogoro ambapo kesi inaunguruma mahakamani hivyo basi hatakiwi mtu yeyote yule kuishi pale. Nyumba hiyo tulikuwa jumla ya wapangaji 2 tu.

Basi ikabidi tumfahamishe sisi tuko pale kihalali na kumuonyesha mikataba yetu ya kupanga, Lakin yeye alidai inabid tuhame tu. Tulichofanya tukampigia yule alietupangisha lakin hakuwa anatoa ushirikiano kwa kusema atatupigia baadae.

Kwahiyo tulichoamua mimi na mpangaji mwenzangu ni kumwita mwenyekiti wa serikali ya mtaa na balozi Ili atusaidie juu ya hilo sekeseke. Kwahiyo tutakaa kikao na hao viongozi tajwa hapo pamoja na mwenye nyumba.
Mwenye nyumba alikiri kumtambua huyo alietupangisha ambaye pia alikuwa anaishi hapo kama muangalizi wa nyumba lakin pia kwa mahusiano ni mtoto wa Babu yake.

Ndugu M/kitu akaamuru yule mwenye nyumba ampigie yule alietupangisha, M/nyumba alipompigia huyo muhusika alietupangisha. Huyo jamaa alipokea simu na alikiri kutupangisha sisi. Na huyo jamaa alietupangisha na muangalizi wa hiyo nyumba lakin pia huyo Mwenye nyumba ni mtoto wa Babu yake kwa uhusiano.

Basi makubaliano ya kikao yalikuwa turudishiwe fedha zetu Ili tuweze kuhama, Sasa Cha kushangaza leo nimerud kwenye shughuli zangu tumekuta mwenye nyumba amekata umeme pamoja na maji. Sasa ndugu zangu nipo njian ya panda nifanyaje.
Naomben ushauri
 
Oya washa botori, chota maji kwa jirani. Hamna kuondoka hapo. Hamna kulipa tena kodi.
Aende yeye mahakamani. Asikuletee utani mpaka upate hela yako. Usiondoke hapo. Tena kama kesi ipo mahakamani hapo kwako, akileta za kuleta ingia nao undugu, waambie ww pia ndugu. Mkatae hadi mwenyekiti. Ila hiyo sio leo. Ww vunga kaa hapo mpaka wakupe chako choteeeee
 
Oya washa botori, chota maji kwa jirani. Hamna kuondoka hapo. Hamna kulipa tena kodi.
Aende yeye mahakamani. Asikuletee utani mpaka upate hela yako. Usiondoke hapo. Tena kama kesi ipo mahakamani hapo kwako, akileta za kuleta ingia nao undugu, waambie ww pia ndugu. Mkatae hadi mwenyekiti. Ila hiyo sio leo. Ww vunga kaa hapo mpaka wakupe chako choteeeee
 
Habari za muda huu?
Nilitafutiwa chumba na dalali maeneo ya Magomen Kagera pale maeneo ya Oil com, Hivyo basi nilitoa kodi ya miez 5 na Kodi ya 1 ya dalali jumla nikatoa tsh 360,000 kwasababu kodi ya chumba ilikuwa tsh 60,000. Sasa baada ya wiki moja alikuja mtu wa makamo na kujitambulisha kuwa yeye ni mwenye nyumba, na hiyo nyumba ni ya kwake alinunua na ipo kwenye mgogoro ambapo kesi inaunguruma mahakamani hivyo basi hatakiwi mtu yeyote yule kuishi pale. Nyumba hiyo tulikuwa jumla ya wapangaji 2 tu.
Basi ikabidi tumfahamishe sisi tuko pale kihalali na kumuonyesha mikataba yetu ya kupanga, Lakin yeye alidai inabid tuhame tu. Tulichofanya tukampigia yule alietupangisha lakin hakuwa anatoa ushirikiano kwa kusema atatupigia baadae. Kwahiyo tulichoamua mim na mpangaji mwenzangu ni kumwita mwenyekiti wa serikali ya mtaa na balozi Ili atusaidie juu ya hilo sekeseke. Kwahiyo tutakaa kikao na hao viongozi tajwa hapo pamoja na mwenye nyumba.
Mwenye nyumba alikiri kumtambua huyo alietupangisha ambaye pia alikuwa anaishi hapo kama muangalizi wa nyumba lakin pia kwa mahusiano ni mtoto wa Babu yake. Ndugu M/kitu akaamuru yule mwenye nyumba ampigie yule alietupangisha, M/nyumba alipompigia huyo muhusika alietupangisha. Huyo jamaa alipokea simu na alikiri kutupangisha sisi. Na huyo jamaa alietupangisha na muangalizi wa hiyo nyumba lakin pia huyo M/nyumba ni mtoto wa Babu yake kwa uhusiano.
Basi makubaliano ya kikao yalikuwa turudishiwe fedha zetu Ili tuweze kuhama, Sasa Cha kushangaza leo nimerud kwenye shughuli zangu tumekuta mwenye nyumba amekata umeme pamoja na maji. Sasa ndugu zangu nipo njian ya panda nifanyaje.
Naomben ushauri
Mkariport serikali za mtaa husika ili aitwe ahojiwe kwani nini amefanya hivyo irihali bado hawa jawarudishia pesa zenu.
 
Oya washa botori, chota maji kwa jirani. Hamna kuondoka hapo. Hamna kulipa tena kodi.
Aende yeye mahakamani. Asikuletee utani mpaka upate hela yako. Usiondoke hapo. Tena kama kesi ipo mahakamani hapo kwako, akileta za kuleta ingia nao undugu, waambie ww pia ndugu. Mkatae hadi mwenyekiti. Ila hiyo sio leo. Ww vunga kaa hapo mpaka wakupe chako choteeeee
Na joto hili bila umeme!
 
Kwanini watu hawapendi kazi za Haki wamezoea utapeli? Kweli alozoea vya kunyonga, kuchinja hawezi. Hao wote lao Moja.
Huenda hata mwenyekiti ana mgao wake, na hapo kapatikana mwingine mwenzio wa kutapeliwa wewe unaonekana unakwamisha maana walidhani ungeondoka haraka uache Kodi bila upinzani. Hiyo nyumba inafuatiliwa kuanzia sasa na sio ajabu wasipate mpangaji Tena milele.
 
Oya washa botori, chota maji kwa jirani. Hamna kuondoka hapo. Hamna kulipa tena kodi.
Aende yeye mahakamani. Asikuletee utani mpaka upate hela yako. Usiondoke hapo. Tena kama kesi ipo mahakamani hapo kwako, akileta za kuleta ingia nao undugu, waambie ww pia ndugu. Mkatae hadi mwenyekiti. Ila hiyo sio leo. Ww vunga kaa hapo mpaka wakupe chako choteeeee
Sawa ndugu
 
Migogoro huwa ipo kwenye haya maisha, Kama mlienda kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa mkawa na kikao, kikaenda vizuri.

Nyie wapangaji mnatakiwa mrudi kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa mtoe taarifa, kisha mpate barua mwende mahakama ya nyumba. Mtasikilizwa na wahusika wataitwa na sio kupigiana simu tena.

Pale mahakamani mtapewa uhalali wa kuishi kwenye hiyo nyumba bila bugudha kwa muda, na wao wanaogombana ikiwa hawana maelewano, au huyo aliyewapangisha kama alifanya makosa mahakama itamuamuru arudishe pesa yenu yote, na mtapewa muda wa kuishi hapo mpaka mtakapo pata nyumba nyingine.

Nyie hamkupewa taarifa za mgogoro wa nyumba uliopo kabla ya kupanga, na mna mkataba hamuhusiki na mgogoro hivyo mta saidiwa kesheria zaidi huko.
 
Nimekosa la kukushauri ila Dunia ni ngumu sana! Tuendelee kumtanguliza Mungu katika mapambano yetu kwenye miji ya watu.
 
Back
Top Bottom