Naomba msaada wa mawazo

Nyalotsi

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2011
Posts
6,986
Reaction score
5,058
Heshima kwenu wakuu. Nina mdogo wangu wa kike amemaliza form four mwaka jana. Amepata four ya 31. Ana D ya chem, bios, maths na kiswahili. Yaliyobaki ana F. Nilipo hapa nawaza asome chuo gani? Nimeangalia nursing wanasema lazima awe na physics na ye aliacha form two. Naomba msaada, kuna chuo cha mambo ya kilimo anachoweza kusoma? Na vyuo vingine ambavyo anaweza kupata nafasi kwa ufaulu wake.
 
Mpeleke cbe,ifm,AIA,TIA,muccobs,saut au tumaini atapokelewa kwa level ya certificate.achana na hayo mambo ya kilimo mkuu.
 
Mpeleke cbe,ifm,AIA,TIA,muccobs,saut au tumaini atapokelewa kwa level ya certificate.achana na hayo mambo ya kilimo mkuu.

huko ataenda kusoma nini? Nataka kozi ambayo haitamfanya awe tegemezi kwenye ajira.
 
huko ataenda kusoma nini? Nataka kozi ambayo haitamfanya awe tegemezi kwenye ajira.

yani mtu kafeli afu bado anachagua chagua kozi!basi mpeleke veta akasomee mapishi.
 
yani mtu kafeli afu bado anachagua chagua kozi!basi mpeleke veta akasomee mapishi.

unajua kuna kozi mtu unasoma aafu unarudi mtaani hakuna cha kufanya. Mfano public administration utamtawala nani? Ndo maana nikafikiria hata kilimo asipopata ajira anaweza kuanza ufugaji au kulima mashamba. Kufeli kusiwe kigezo cha kumpeleka mtu hata vyuo ambavyo ni vya kisanii mkuu.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…