Ndugu wna jamvi mambo ya kisheria na taratibu zke naomba msaada
nilikuwa namdai mtu kumbe anatumia njia za kihuni kutapeli pesa za watu sasa nimezunguka na kujua jamaa kaoa na katika kutaka kukmkamata kakimbia swali je ni haki kumkamata mke wake ili yeye aweze kurudi? Kisheria na kawaida
naomba msaada wenu wana jamvi hili
Mkuu, huwezi kumkamata mke wake kwa kuwa siye unamtuhumu kukutapeli. Wewe toa taarifa polisi wamtafte mmewe ambaye ni muhusika. Ukimkamata mkewe kisa mumewe kakutapeli anaweza kuja kukufungulia kesi ya 'unlawful imprisonment'. Angalia mkuu.