Naomba mwangaza kuhusu biashara ya “Mineral brokering”

leonce100

Member
Joined
Jun 8, 2019
Posts
5
Reaction score
2
habari wana JF!
nina mtaji wa kiasi fulani cha fedha nataka nijikite katika masuala ya mineral brokering maana ni biashara nayoipenda sana. napenda kufahamu some ABC's kuhusu hii biashara. yaani kulangua madini na kuyauza kwa faida.
 
Kama upo tayari nenda mkoa wa Geita ukifika anza taratibu upate uzoefu ikiwezekana anzia chini kabisa ujue madili yanavyochezwaga ukikomaa ndio unaanza biashara nyingi haziko nyepesi kama unavyoziona....
Kama hauko tayari kufanya mambo ya kwenda kwa waganga achana na hiyo biashara hutoiweza inahitaji nguvu kutoka ndani madini, samaki sio biashara za watu dhaifu.
 
asante sana mkuu, ngoja nilifanyie kazi. ngoja nitakwenda Geita nikapate mauzoefu kwanza.
 
madini mbalimbali kama dhahabu, alimasi n.k

Kwa dhahabu itakua ngumu sana
Kwako kwasbb makota wote wa dhahabu huwa wanakatabia ya kuchanganya na kakumba,vilevile soko la dhahabu lipo wazi na kujulikana bei yake ulimwenguni,hata kama utapata faida itakua ni ndoogo saana
Lkn kwa almasi hapo nakuunga mkono ila kuwa makini saana na ma broker wa maganzo,wale neno lao la kuwaamini ni salamu tu,mengineyo yote usiwaamini
Notice-Almasi kama haufahamu nakushauri ujifunze kwanza kabla ya kuingilia hio biashara,usije ukalia kilio cha mbwa mwitu
 
asante mkuu kwa maelekezo, maana mtu unaweza lia kilio cha mbwa mwitu kabisa,,,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…