Naomba nieleweshwe hili

Pennsylvania

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2019
Posts
335
Reaction score
503
Habari wote humu,

Niende moja kwa moja kwenye mada.

Kuna kisiwa kinaitwa "Fungu Yasini", Nimeona picha zake nimevutiwa nacho kukitembelea ukizingatia ku fanya "voyages" ni DNA yangu.

Nimefika Mbudya, Bongoyo, Zanzibar, Dolphin island, Prison Island, Nungwi, Chakwani, Paje.

Nisiwachoshe wakuu, ninachohitaji ni jinsi gani naweza kufika (direction).

Nimeangalia kwenye Map kipo mbali kidogo, tofauti na Mbudya na Bongoyo.

Karibuni kwa michango yenu ya jinsi ninavyoweza kufika.

Hizo chini ni picha za kisiwa cha "Fungu Yasini".

 
Hakuna aliyefika hichi Kisiwa au mwenye Taarifa zake?
 
Inaoneka ni vile visiwa ambavyo vinakuwepo kwa muda wa masaa kadhaa tu ya siku. Yaani kuna muda hufunikwa na maji.
 
Nahitaji kwenda Mbudya au Bongoyo hii Nov... Mkuu waeza nisaidia gharama zilivyo currently na njia rahisi ya kufika huko. Ukitokea mjini/kariakoo
 
Nahitaji kwenda Mbudya au Bongoyo hii Nov... Mkuu waeza nisaidia gharama zilivyo currently na njia rahisi ya kufika huko. Ukitokea mjini/kariakoo
Mbudya Nilipanda Escape two, Mbezi beach.

Gharama ilikuwa 15k each person. ( Kwenda na kurudi).

Bongoyo Nilipanda msasani. (To and fro) 20k.

Mbudya kuzuri mno, maji ni ya Sky blue, white powdery sand hadi raha, pia kama ni mpenzi wa picha, hapo ndio penyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…