Naomba TANROADS waweke bango la kuelekea watumia barabara badala ya kujitangaza wao

DENAMWE

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2019
Posts
862
Reaction score
871
Nimeona mabango mengi yaliyowekwa na TANROADS kwa ajili ya tahadhari yanatanguliwa na maneno yenye herufi kubwa yahusuyo TANROADS badala ya kujikita kwenye kutoa tahadhari.

Naomba wafikirie kuandika au kuweka maneno na michoro ya kutoa tahadhari badala ya wao kujitangaza.

Hii ina maana kuwa bango linajaa maneno mengi yasiyohitajika.
Namaanisha maneno yahusuyo TANROADS hayatoi tahadhari.

Iwapo inaonekana ni lazima jina au neno lao liwepo basi nashauri liwekwe chini kwa maandishi madogo.
 
Isomeke kuelekeza badala ya kuelekea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…