Naomba ufafanuzi juu ya kutofautiana kwa majina ya mtu mmoja katika vyeti viwili

Naomba ufafanuzi juu ya kutofautiana kwa majina ya mtu mmoja katika vyeti viwili

raphalena

Member
Joined
Oct 2, 2011
Posts
32
Reaction score
4
Habari ya leo kaka na dada zangu mlio ndani ya jukwaa hili la sheria, mimi ninahitaji ufafanuzi na ushauri iwezekanavyo, juu na tofauti ya majina katika vyeti viwili ambavyo vinakuwa ni vya mtu mmoja.
mimi ninasoma Korea Kusini, Undergraduate yangu nimesoma UDOM na nilikuwa natumia majina mawili (LEONARD Raphael) ambayo pia ni majina ambayo nimekuwa nikitumia secondari, lakini wakati naomba scholarship, application form yangu ya chuo ilinitaka nitumie majina kama yanavyoonekana katika Passport yangu ya kusafiria ambayo ina majina matatu (TILUHONGELWA Raphael Leonard) pia ndo majina yanayoonekana katika cheti changu cha kuzaliwa.
Tofauti iliyopo hapa ni kuongezeka kwa jina la tatu katika cheti changu cha Masters ambacho kitakuwa tofauti na cheti cha Undergraduate.
Kutokana na hili naomba ufafanuzi, Je kutokana na tofauti hii yaweza kuniletea matatizo nimalizapo masomo yangu huku nirudipo Tanzania hasa katika utafutaji wangu wa ajira?, na kama inaonekana kutokukubalika kisheria, kunaumuhimu wa mimi kupata kiapo cha Kisheria (mahakama/wakiri) ili kuweza kuthibitisha kuwa vyeti vyote vihili ni vya mtu mmoja? na kama nitatakiwa niwe na kiapo hicho cha kisheria, nitatakiwa katika kila maombi yangu ya ajira niambatanishe kiapo hicho?
au ninatakiwa nifanye jitihada zingine za kufanya vyeti vyote viwili viwe na majina yanayofanana either majina mawili kama kilivyo cha UDOM ama majina matatu kama kilivyo cha Masters?
 
mimi binafsi sioni tatizo lolote lile hapo..na hakika wakati unaaply huko udom kuna sehem ulijaza hilo jina la tatu..so whatever the case might be utatambulika tu..as long as wewe ni holder wa hicho cheti...nafikiri baada ya hapo umeshajifunza faida na hasara za kutumia majina mawili ambayo yote ni ya kiingereza..over..!!!
 
Asante sana kaka Lyamber kwa maelezo yako nikweli nimejifunza katika hilo na tatizo lenyewe ni hii mifumo yetu ya uandikishwaji wa majina tunapoanza elimu ya awali, maana mifumo yetu ya awali inaturuhusu mtoto kuanza shule ya msingi kwa majina mawili hivo kupelekea kuingia katika mfumo kwa majina mawili halafu inapofikia katika baadhi ya mambo kama vyeti vya kuzaliwa na passport tunahimizwa majina matatu hivyo kupelekea kuwepo kwa tofauti katika vyeti ambavyo vinakuwa vya mtu mmoja
 
unahitaji deep poll, ungekuwa hapa dsm ningekutengenezea fasta. sasa upo korea...dah...nimekosa ulaji hapo. try to consult tz embassy in Seoul if they have a state attorney at the embassy au namna gani unaweza ku arrange kufanya hiyo kitu, au kama hicho chuo wanaweza kukusaidia uendelee na masomo lakin next term ukirudi likizo urudi na kiapo kuwa majina hayo yote ni ya kwako hata kama sehemu nyingine yapo mawili na nyingine matatu...kiapo hicho lazima kiwe na mhuru wa commissioner for oath, and i am one of them.
 
Back
Top Bottom