Naomba ufafanuzi kuhusu hiliu joto la engine ya gari

Meja M

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2016
Posts
628
Reaction score
560
Wataalam habari za wakati huu! Poleni na majuku yenu ya kila siku.

Naomba kujuzwa je ni sahihi joto la engine ya gari kuwa 108 degree centigrade then linashuka hadi 106 hapo nikiwa naendesha sasa naombeni kujua kama hili joto ni kawaida au kuna shida mahala.

ASANTE
 
Hiyo ni kawaida ukiona unaitafuta 120 ndio balaa.
 
Gari yangu haionyesho joto la gari ila naendesha tu!
 
jamani joto la gari mnaangalizia wapi?mimi yangu ina,,mshale wa kuonyesha C au H.
 
Wenzangu naona mna magari ya mwaka 47
Magari mengi yenye cc 1500 kushuka chini ndo hua hayaoneshi C na H mkuu yako inaonesha ikiwa imewaka ni kile kitaa cha bluu sasa hio kama inashinda ya cooling system unaistukia imewaka nyekundu na gari kuzima wakati magari mengine unaona inavyopanda tuu kwaio unastuka
 

kuna gari kama bmw 3 series ya 2005 haina kabsa temperature gauge mkuu, wala haina hicho kitaa cha blue ili kupata temp yake lazima uaunlock code za temp ndo unaweza ona temp yake
 
kuna gari kama bmw 3 series ya 2005 haina kabsa temperature gauge mkuu, wala haina hicho kitaa cha blue ili kupata temp yake lazima uaunlock code za temp ndo unaweza ona temp yake
Hata baadhi ya VW kama Amarok. Nazo zina taa tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…