Naomba ufafanuzi kuhusu TIN number na Leseni

Joined
Nov 4, 2015
Posts
23
Reaction score
1
Habari zenu wajasiriamali,

Hivi kati ya lesseni na tini kipi kinaanza, Na lesseni inapatikana wapi na tini inapatikana wapi, au vyote vunapatikana TRA.
 
Habari zenu wajasiriamali,

Ivi kati ya lesseni na tini kipi kinaanza ,

Na lesseni inapatikana wapi na tini inapatikana wapi, au vyote vunapatikana TRA
 
Habari zenu wajasiriamali,

Ivi kati ya lesseni na tini kipi kinaanza ,

Na lesseni inapatikana wapi na tini inapatikana wapi, au vyote vunapatikana TRA
Tin namba ndio inaanza, kwanza nayo inapatikana ktk ofisi ya TRA, iliyopo karibu na eneo lako la biashara unayotaka kufungua, na ni bure bila malipo, kabla ya kwenda tra, nenda ofisi ya serikali ya mtaa wako, wakupe barua ya utambulisho kwanza, japo kuna sehemu unaanzia tra, watakupa fomu ndio ujaziwe na s, za mitaa yaani huwa hawaeleweki, ila anzia serikali ya mtaa. Huko tra ndio utaaja ni biashara gani unafungua, na kiasi cha mtaji, watakukadiria kodi, ambayo wanaigawa kwa installment 4,kulingana na kiwango chake. Ila lazima siku hiyo ulipe installment ya kwanza, ndio una pata tin number, hapo sasa unaanza mchakato wa leseni itabidi uende ofisi ya halmashauri na copy ya hiyo tin number, utajaza form huko, na kulipia hiyo leseni baada ya muda utapata leseni yako.
 
Tin no ndo inaanza then unaenda nayo kwa afisa biashara siku hizi inaambatishwa na kitu kinachoitwa tax clearance, ushahidi kuwa huna deni la kodi then unapewa leseni baada ya maafisa mbalimbali wa halmashauri ku endorse
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…