Naomba ufafanuzi kutoka kwa Dr. Ndalichako na Waziri Kawambwa kuhusu matokeo kidato 4 2012

Naomba ufafanuzi kutoka kwa Dr. Ndalichako na Waziri Kawambwa kuhusu matokeo kidato 4 2012

Njaare

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2010
Posts
1,081
Reaction score
275
Wana Jamvi,

Ninamwomba Dr. ndalichako anipe ufafanuzi kuhusu mambo ambayo nitayaeleza. Ni mawazo yangu binafsi ila yananikera.

Dr Ndalichako alinifundisha somo linaitwa educational measurement and evaluation chuo kikuu cha Dar es Salaam pamoja na prof Issa Omari. Alikuwa mahiri sana kwenye hilo somo na alikuwa anasisitiza kuwa kama mtihani umetungwa vizuri, matokeo yatakuwa na mtawanyiko mzuri (normal distribution). La kushangaza bado hajatoa maelezo ya kuridhisha (Analysis) kwa nini matokeo ya mwaka huu yamelalia zaidi upand wa kufeli (skewed to the left).

Kuna sababu mbili haya matokeo kuwa hivi. Ya kwanza ni kuwa wanafunzi hawakufundishwa au ni kuwa mtihani haukuwa umetungwa kitaalamu. Mimi siamini kuwa wanafunzi wote hawakufundishwa. Baadhi ya shule wamefundishwa vizuri hivyo kwa shule hizo matokeo yangeonyesha normal distribution. hata hivyo hili halikuonekana jambo ambalo linaonyesha kuwa kuna matatizo mengine.

Kwa vile matokeo hata kwa shule zilizokuwa na walimu yanaonyesha kuwa ni skewed to the left, inaonekana kuwa baraza chini ya Dr. Ndalichako ama lilitunga mtihani nje ya mihutasari ya masomo (syllabus) au usahihishaji wa mitihani haukuwa makini au uingizaji wa matokeo haukuwa sahihi.

Dr Ndalichako, Hebu tuambia kati ya haya nilioeleza ndio sababu ya kufeli kwa hawa watoto? Najua kwa swali hili utapata kigugumizi maana najua hakika unajua sababu.

Mimi ninafikiri kati ya haya yafuatayo yalitokea.

Kwanza naomba nikumbushe mgomo wa walimu uliotokea mwaka jana na miaka ya nyuma. Walimu walisema kuwa wameamuriwa kurudi kazini na mahakama. wakazidi kulalama kuwa pamoja na kuwa wamelazimishwa kurudi kazini, watarudi ila mgomo unaendelea. Je haiwezekani kuwa walimu walichangia?

Pili, ukosefu wa walimu na vitabu katika shule za kata. Wanafunzi hawakufundishwa na hata pale walipotaka kujisomea hawakuwa na jinsi ya kujisaidia.

Kutokana na mambo mawili hayo hapo juu, waziri anaweza akawa alichakachua matokeo na kushusha viwango vya ufaulu kwa shule binafsi zenye walimu na vitabu ili wananchi waone kuwa ni wanafunzi wote walifeli. Hii inanipa wasiwasi kwa sababu waziri na Ndalichako wamekuwa wakisisitiza kuwa hata wanafunzi wa private nao wamefeli! Vile vile wasiwasi wangu unatokana na sababu kuwa mwenye mamlaka ya kutangaza matokeo ni katibu mtendaji wa baraza. Iweje waziri ayatangaze? Ni lini sheria ilibadilika?

Tatu, Posho kidogo wanayopewa walimu wanaosahihisha mitihani hivyo kutokuwa makini katika usahihishaji.

Nne, Copy and Paste
 
Kwa kuangalia habari mbalimbali kuhusu huku kufeli kwa wanafunzi wengi( hawa form4 wa mwaka huu), mimi nadhani Ndalichako hana cha kulaumiwa.

Wanafunzi ambao shule zao zina walimu wakueleweka na zina fedha na zina nyezo za kufundishia, wanafunzi wamefaulu vizuri. Tatizo lipo katika uwajibikaji wa wizara ya elimu sio baraza la mitihani.

Kitu ambacho kinanipa mashaka ni kwamba serikali ina shule nyingi sana za O-levels(+ za kata) ambazo hazina uwiano na nafasi za A-levels, na kawaida div I na div II ni lazima wapewe nafasi kwenye shule za serikali.
Je ni lipi bora kwa siasa za serikali yetu: ni bora kuchakachua matokeo na kufaulisha kulingana na uwezo wa serikali kusomesha(ili wengine wakajilipie private schools) au kuacha wengi wafaulu lakini serikali iingie kashfa kuwa wameshindwa kusomesha wanafunzi waliofaulu?
Kucheleweshwa kidogo kwa matokeo ya form four lazima kuna adjustment iliyokuwa inafanyika.
 
Heheeeeeeee wewe unaomba mwongozo kwa asiyejua kazi yake?. Umelogwa au?
 
Kuna sababu mbili haya matokeo kuwa hivi. Ya kwanza ni kuwa wanafunzi hawakufundishwa au ni kuwa mtihani haukuwa umetungwa kitaalamu. Mimi siamini kuwa wanafunzi wote hawakufundishwa. Baadhi ya shule wamefundishwa vizuri hivyo kwa shule hizo matokeo yangeonyesha normal distribution. hata hivyo hili halikuonekana jambo ambalo linaonyesha kuwa kuna matatizo mengine.

Kwa vile matokeo hata kwa shule zilizokuwa na walimu yanaonyesha kuwa ni skewed to the left, inaonekana kuwa baraza chini ya Dr. Ndalichako ama lilitunga mtihani nje ya mihutasari ya masomo (syllabus) au usahihishaji wa mitihani haukuwa makini au uingizaji wa matokeo haukuwa sahihi.

Mimi ninafikiri kati ya haya yafuatayo yalitokea.

Kwanza naomba nikumbushe mgomo wa walimu uliotokea mwaka jana na miaka ya nyuma. Walimu walisema kuwa wameamuriwa kurudi kazini na mahakama. wakazidi kulalama kuwa pamoja na kuwa wamelazimishwa kurudi kazini, watarudi ila mgomo unaendelea. Je haiwezekani kuwa walimu walichangia?

Pili, ukosefu wa walimu na vitabu katika shule za kata. Wanafunzi hawakufundishwa na hata pale walipotaka kujisomea hawakuwa na jinsi ya kujisaidia.

Vile vile wasiwasi wangu unatokana na sababu kuwa mwenye mamlaka ya kutangaza matokeo ni katibu mtendaji wa baraza. Iweje waziri ayatangaze? Ni lini sheria ilibadilika?

Tatu, Posho kidogo wanayopewa walimu wanaosahihisha mitihani hivyo kutokuwa makini katika usahihishaji.

Nne, Copy and Paste

Nimejaribu kupitia makala yako kwa karibu zaidi na kubaini kuwa unachokieleza hukijui. Yaani kwa maneno mengine unalopoka (unabwabwaja kijana). Huna mashiko katika hoja zako, ama uelewa wako (comprehension) wa statistics uliofundishwa na Dr. Ndalichako ni finyu (surface knowledge). Kama unafahamu sababu zipelekeazo kufeli wanafunzi kama ulivyo ainisha unamtaka Dr. Ndalichako aseme nini? Skewness? unaposema zipo shule zilifundisha vizuri, Je, unauthibitisho wa ubora wa ufundishaji katika shule hizo? Hebu tueleze mifano ya shule zilizofundisha vizuri ufahamuvyo wewe na vigezo gani vilivyokuthbitishia uzuri au ubora wa ufundishaji ktk shule hizo. Je, unajuwa muundo wa usahihishaji unavyofanyika au unaleta porojo na siasa hata mahala pasipo hitaji siasa? Je, kunauhusiano gani kati ya Shukuru Kawambwa kutangaza matokeo na kufeli kwa wanafunzi? Kijana acha kuwa kama bongo-lala au umetumwa na watu kuleta hoja butu?
 
Kwa kuangalia habari mbalimbali kuhusu huku kufeli kwa wanafunzi wengi( hawa form4 wa mwaka huu), mimi nadhani Ndalichako hana cha kulaumiwa.

Wanafunzi ambao shule zao zina walimu wakueleweka na zina fedha na zina nyezo za kufundishia, wanafunzi wamefaulu vizuri. Tatizo lipo katika uwajibikaji wa wizara ya elimu sio baraza la mitihani.

Kitu ambacho kinanipa mashaka ni kwamba serikali ina shule nyingi sana za O-levels(+ za kata) ambazo hazina uwiano na nafasi za A-levels, na kawaida div I na div II ni lazima wapewe nafasi kwenye shule za serikali.
Je ni lipi bora kwa siasa za serikali yetu: ni bora kuchakachua matokeo na kufaulisha kulingana na uwezo wa serikali kusomesha(ili wengine wakajilipie private schools) au kuacha wengi wafaulu lakini serikali iingie kashfa kuwa wameshindwa kusomesha wanafunzi waliofaulu?
Kucheleweshwa kidogo kwa matokeo ya form four lazima kuna adjustment iliyokuwa inafanyika.

Hapo kwenye nyekundu nikukumbushe hakuna shule hata moja ya private ambayo imefanya vizuri,kua na Dv1 siyo sababu ya kuona imefanya vizuri.
 
Nimejaribu kupitia makala yako kwa karibu zaidi na kubaini kuwa unachokieleza hukijui. Yaani kwa maneno mengine unalopoka (unabwabwaja kijana). Huna mashiko katika hoja zako, ama uelewa wako (comprehension) wa statistics uliofundishwa na Dr. Ndalichako ni finyu (surface knowledge). Kama unafahamu sababu zipelekeazo kufeli wanafunzi kama ulivyo ainisha unamtaka Dr. Ndalichako aseme nini? Skewness? unaposema zipo shule zilifundisha vizuri, Je, unauthibitisho wa ubora wa ufundishaji katika shule hizo? Hebu tueleze mifano ya shule zilizofundisha vizuri ufahamuvyo wewe na vigezo gani vilivyokuthbitishia uzuri au ubora wa ufundishaji ktk shule hizo. Je, unajuwa muundo wa usahihishaji unavyofanyika au unaleta porojo na siasa hata mahala pasipo hitaji siasa? Je, kunauhusiano gani kati ya Shukuru Kawambwa kutangaza matokeo na kufeli kwa wanafunzi? Kijana acha kuwa kama bongo-lala au umetumwa na watu kuleta hoja butu?


Jibu hoja kwa kutoa hoja siyo kumlaumu mleta mada bila wewe kuonyesha hayo unayoyajua,anayeropoka ni wewe kama vile umetoka usingizini!
 
hata wakirudia mtihani ninauhakika watafeli hivihvi tu!!!!
 
Mtoa mada amechambua vizuri sana ila inapotoke watu wanamkejeli na kumkosoa bila na wao kujenga hoja zao
inaleta mashaka kama watu wanatumia ubongo kufikiri.
Yeye ameeleza fikra zake kuwa anafikiri kile alichokieleza ndio kimesababisha,
Hivyo ingekuwa busara kama na we ungeeleza kile unachokifahamu.
 
Nimejaribu kupitia makala yako kwa karibu zaidi na kubaini kuwa unachokieleza hukijui. Yaani kwa maneno mengine unalopoka (unabwabwaja kijana). Huna mashiko katika hoja zako, ama uelewa wako (comprehension) wa statistics uliofundishwa na Dr. Ndalichako ni finyu (surface knowledge). Kama unafahamu sababu zipelekeazo kufeli wanafunzi kama ulivyo ainisha unamtaka Dr. Ndalichako aseme nini? Skewness? unaposema zipo shule zilifundisha vizuri, Je, unauthibitisho wa ubora wa ufundishaji katika shule hizo? Hebu tueleze mifano ya shule zilizofundisha vizuri ufahamuvyo wewe na vigezo gani vilivyokuthbitishia uzuri au ubora wa ufundishaji ktk shule hizo. Je, unajuwa muundo wa usahihishaji unavyofanyika au unaleta porojo na siasa hata mahala pasipo hitaji siasa? Je, kunauhusiano gani kati ya Shukuru Kawambwa kutangaza matokeo na kufeli kwa wanafunzi? Kijana acha kuwa kama bongo-lala au umetumwa na watu kuleta hoja butu?

Ukweli unauma enh"!!! tangu lini waziri anatangaza matokeo,ni suala la muda tu yote yaliyo behind the scene
yatakuwa wazi" Mleta mada yuko sahihi"jibu hoja acha kutoka povu"
 
Nimejaribu kupitia makala yako kwa karibu zaidi na kubaini kuwa unachokieleza hukijui. Yaani kwa maneno mengine unalopoka (unabwabwaja kijana). Huna mashiko katika hoja zako, ama uelewa wako (comprehension) wa statistics uliofundishwa na Dr. Ndalichako ni finyu (surface knowledge). Kama unafahamu sababu zipelekeazo kufeli wanafunzi kama ulivyo ainisha unamtaka Dr. Ndalichako aseme nini? Skewness? unaposema zipo shule zilifundisha vizuri, Je, unauthibitisho wa ubora wa ufundishaji katika shule hizo? Hebu tueleze mifano ya shule zilizofundisha vizuri ufahamuvyo wewe na vigezo gani vilivyokuthbitishia uzuri au ubora wa ufundishaji ktk shule hizo. Je, unajuwa muundo wa usahihishaji unavyofanyika au unaleta porojo na siasa hata mahala pasipo hitaji siasa? Je, kunauhusiano gani kati ya Shukuru Kawambwa kutangaza matokeo na kufeli kwa wanafunzi? Kijana acha kuwa kama bongo-lala au umetumwa na watu kuleta hoja butu?



Lazima wewe ni kawambwa au umetumwa na kawambwa, chanzo kikuu cha kufeli kwa wanafunzi ni kawambwa si Ndalichako, kumbuka majibu ya katibu wa chama cha walimu aliposema hili ndo jibu kwa serikali kupuuza madai ya walimu.
 
Back
Top Bottom