Naomba ufafanuzi nikifanya kosa hili itakuwa kesi ya aina gani?

Naomba ufafanuzi nikifanya kosa hili itakuwa kesi ya aina gani?

Manjagata

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2012
Posts
13,942
Reaction score
15,371
Kutokana na wimbi la CORONA sasa hivi ofisi nyingi zimefungwa na raia wanafanyia kazi majumbani! Sasa juzi kati nimepata deal kutoka ofisi nyingine wanataka waniajiri. Sasa nikawa nawaza kwa sauti kwa vile mwajiri wangu yuko kwenye mchakato wa kufunga ofisi jumla muda si mrefu, nikapata kishawishi cha kukubali hiyo ajira ambayo yenyewe itakuwa ya muda mrefu.

Sasa huyu mwajiri wangu wa zamani anayeondoka nikaamua nimpige cha juu yaani niwe navuta mishahara miwili kwa kipindi kilichobaki. Sasa nauliza hapo nikidakwa naweza kuwa natenda kosa la jinai? Na nikikamatwa itakuwa kesi ya aina gani hii, uhujumu uchumi au utakatishaji fedha?

Tuongezeane maarifa wadau maana tozo nazo zimekuwa nyingi sana!
 
Fanya kazi kwa uaminifu kote kuwili. Wajapani wanafanya kazi masaa 17 kwa siku.
 
Usichanganye changanye, unatakiwa uwe makini sana , lkn pia ucmwambie yeyote zaid ya humu jf, ukimweleza mtu anakwenda kukuchomea kwa boss na kama boss wako mtu wa majungu atakupa kazi nyiiiiingi ili ukose muda wa kufanya kazi kwingine
 
Utakuwa na makosa mawili na utafungwa kwenye jela mbili wiki hii unalala gereza hili wiki inayokuja unaenda kulala gereza lingine mzunguko utakuwa ndio huohuo mpaka umalize vifungo
 
Utakuwa na makosa mawili na utafungwa kwenye jela mbili wiki hii unalala gereza hili wiki inayokuja unaenda kulala gereza lingine mzunguko utakuwa ndio huohuo mpaka umalize vifungo
Yatakuwa makosa gani?
 
Back
Top Bottom